Tuesday 31 May 2016

WANANCHI WA MKOA WA GEITA BADO HAWAELEWI MIRADI MBALIMBALI INAYOANZISHWA NA MGODI WA DHAHABU WA GEITA(GGM)


Mkuu  wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga   amesema kuwa  miradi mbalimbali inayoanzishwa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), bado haieleweki kwa Wananchi hali ambayo inasababisha kuwepo kwa malalamiko mengi.
Kyunga  ametoa  kauli hiyo  wakati  akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa kikao cha kujadili   namna ambavyo  halmashauri  ya wilaya na mji geita watakavyoweza kuwashirikisha  Wananchi katika  miradi inayoanzishwa  na Mgodi  huo.

Amesema  kuwa  imefikia hatua  Wananchi wanautuhumu mgodi huo kuwa   hauna   manufaa yoyote kwao jambo ambalo limewalazimu kuketi kujadili   baadhi  ya mambo yatakayoeleweka  kwa jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Marx Kamaoni amesema kuwa miongoni  mwa matumizi yaliyofanyika kutokana na fedha  za  ushuru  wa huduma    kwa  jamii  zilizotolewa na Mgodi (service levy)  zimenunulia mitambo ya kutengenezea barabara    iliyogharimu kiasi cha Sh.Bilioni 1.2.


Hata hivyo kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa baadhi ya madiwani wa halmashauri   zote  mbili kupinga  utaratibu uliowekwa na halmashauri  hizo  kuwa atakayetaka   kurekebisha  miundombinu katika eneo  analotoka aweke mafuta kwa gharama zake.

No comments:

Post a Comment