Tuesday 16 February 2016

WAFANYAKAZI WA TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA KUANZA KUJISAFISHA.


       
          Waziri wa nchi, ofisi ya rais, utumishi na utawala bora, Mh  Angela Kairuki.

Wafanyakazi wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na  rushwa (takukuru), wametakiwa  kuanza kujisafisha  huku wakiambiwa kwamba taasisi hiyo  haitaepuka kutumbuliwa  majipu.
Aidha, wameagizwa kuwasilisha upya taarifa za mali zao kwa sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma, zifanyiwe uhakiki wa mali; moja baada ya nyingine kubaini waliofanya udanganyifu wa umiliki wa mali zao.
Waziri wa nchi, ofisi ya rais, utumishi na utawala bora, Mh  Angela Kairuki amesema hayo jijini  dar es salaam kwenye ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa viongozi wa taasisi hiyo.
Aidha amesisitiza kuwa tayari anazo taarifa zinazohitaji baadhi ya viongozi wa taasisi hiyo kutumbuliwa majipu muda muafaka utakapowadia.
Mh Kairuki ameagiza taasisi hiyo kufanyia tathmini kesi zake zote, ilizowahi kushindwa na kuja na majibu ya sababu za kushindwa na endapo itabainika hazikushinda kutokana na mchezo mchafu wa wachunguzi, wahusika wachukuliwe hatua haraka iwezekanavyo.

Amesema iwapo yupo mtumishi hasa viongozi wa taasisi hiyo, anayejitambua kuwa ni ‘jipu’, ajisalimishe kwani akiendelea kusubiri na kutumbuliwa, mwisho wake utakuwa mbaya.

No comments:

Post a Comment