Saturday 16 April 2016

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA DKT.MWAKYEMBE KATIKA ZIARA YA SIKU MOJA MKOANI GEITA


Serikali imekiri kuwepo kwa mlundikano mkubwa wa watu katika magereza huku sababu ikielezwa ni ucheleweshwaji wa kesi unaosababishwa na kucheleweshwa  kwa kesi za baadhi ya washitakiwa.

Akizungumza na watendaji wa Serikali mkoani Geita katika ofisi za mkuu wa mkoa,Waziri wa katiba na sheria, Dkt. Herson Mwakyembe amesema kuwa  kutokana na kucheleweshwa kwa kesi hali hiyo imekuwa ikisababisha kuwepo kwa mlundikanao mkubwa wa watu hali ambayo imeendelea kutishia usalama  wa  afya kwa baadhi  ya wafungwa.

Akitoa taarifa ya Wkoa  kwa Waziri Mwakyembe Mkuu wa Wilaya  ya Geita, Mh.Manzie Manguchie amesema kuwa mkoa wa Geita unakabiliwa na uhaba wa gereza la mkoa hali ambayo kumekuwa na changamoto  ya watu kuwa wengi katika magereza.

Aidha waziri Mwakyembe amewata wananchi mkoani hapa kubadilika na kuachana  na vitendo vya imani  za kishirikina za mauaji  dhidi ya  watu wenye  ulemavu wa ngozi  (zeruzeru) huku akiitaja mikoa ya Mwanza,Mara na Geita kuongoza kwa mauaji hayo.

Waziri Mwakyembe amefika asubuhi na mapema leo akitokea jijini Mwanza  na yupo mkoani Geita  kwa ziara ya siku moja ambapo atatembelea,Ofisi ya Mwanasheria mkuu,Ofisi ya vizazi na vifo (RITA) na  kuzungumza na wafungwa katika gereza  la wilaya ya Geita.


No comments:

Post a Comment