Tuesday 5 April 2016

MVUA NA NGUZO ZA TANESCO ZAWA SABABU YA BARABARA YA JIMBONI MKOANI GEITA KUCHELEWA KUKAMILIKA.

Mvua na nguzo za Tanesco kuwa ndani ya barabara ya jimboni mkoani Geita  ni sababu ambazo zimepelekea kuchelewa kukamilika kwa wakati ujenzi wa barabara hiyo yenye  kilomita 2.2.


Mkuu wa mkoa wa geita meja jenereali mstaafu Ezekiel Kyunga ameeleza sababu hizo ofisini kwake  wakati akizungumza na Storm habari  kufuatia malalamiko yaliyotolewa na mbunge wa jimbo la Geita vijijini mh Joseph Msukuma hivi karibuni katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari Chato mbele ya Rais wa Tanzania dk. John Pombe Magufuli, ambapo mbunge huyo alidai kuwa mkandarasi  wa kampuni ya Jasco ya jijini Mwanza anayejenga barabara hiyo ameshindwa kukamilisha kwa wakati.

Mh kyunga, amesema zipo sababu za msingi zilizochelewesha barabara hiyo ambapo baadhi ya mambo yaliyokwamisha kutokamlika kwa ujenzi wa barabara hiyo ni pamoja na mvua ambazo zinaendelea kuyesha mkoani Geita.

Katika hatua nyingine mh Kyunga amesema kuwa katika kikao cha RCC kilicho keti  mwezi disemba mwaka jana chini ya mkuu wa mkoa  aliyekuwepo bi. Fatuma Mwassa  waliingiwa na wasiwasi juu utekelezaji wa mradi   huo.

Aidha kwa upande wao wananchi wamepongeza kwa ujenzi wa barabara hiyo kuwa kiwango kinachotumika kwa kujenga ni cha uhakika huku wakimwomba mkandarasi huyo kupanua zaidi.

Barabara  hiyo inayofadhiliwa na benki ya dunia, ujenzi wake ulianza mwezi julai mwaka jana na  unatarajia kukamilika mwezi huu licha ya chanagmoto zilizopo katika kukamilisha mradi huo,  huku barabara hiyo ikisubiriwa kwa hamu na wananchi kwani itaondoa kero  na  adha  zilizopo.

No comments:

Post a Comment