Wednesday 13 April 2016

MAJAMBAZI YAUAWA KAHAMA YAKIWA NA SILAHA ZA KIVITA.






Jeshi la Polisi wilayani Kahama mkoani Shinyanga limefanikiwa kuwauwa Majambazi watatu katika Majibizano ya Risasi,huku moja likifanikiwa kutoroka kwa kutumia Pikipiki ambayo haikuwa na usajili.


Tukio hilo limetokea jana April 12 majira ya saa 12 jioni katika Mtaa wa Msikiti mkuu ,barabara ya Tabora mjini Kahama ambapo Majambazi hao wakiwa na silaha za moto.

Taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani shinyanga iliyotolewa na kusainiwa na kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga Dismas Kisusi kwa niaba ya kamanda wa Polisi mkoani humo Mika Nyange imeeleza kuwa mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina la Emmanuel mkumbo mfanyabiashara wa bidhaa za jumla mjini Kahama alivamiwa na kupigwa risasi kifuani na kichwani baada ya kukaidi agizo aliloamrishwa na majambazi hao la kuwapatia fedha

Mbali na mfanyabiashara huyo kuuawa mpita njia aliyefahamika kwa jina la Seleman Shaban alipigwa risasi na majambazi hayo yakiwa katika majibizano ya Risasi na Jeshi la Polisi ambapo alipata majeraha na kukimbizwa katika Hospitali ya wilaya ya Kahama ambapo amefariki akiwa anapatiwa matibabu.

Katika tukio hilo Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata silaha mbalimbali za kivita zilizokuwa zikitumiwa na Majambazi ambazo ni pamoja na Bunduki aina ya SMG yenye namba za usajili 1996-AFU 2297,bunduki aina ya UZIGUN yenye namba za usajili 3452, Magazini 3 za SMG, Risasi 30 zinazotumika katika bunduki ya SMG na Risasi zingine 30 za UZIGUN, Mabomu mawili ya kurushwa kwa mkono na Kisu kimoja cha kijeshi.
Vitu vingine vilivyokamatwa ni Pikipiki mbili, moja aina ya SanLG namba zake za usajili ni T959 CAE yenye Chesis namba LBRSPJ51C900191,na nyingine ambayo haikuwa na namba za usajili  ikiwa imefutwa namba za Chesis

Katika uvamizi huo Majambazi hawakufanikiwa kuchukua kitu chochote na Jeshi linaendelea kumtafuta Jambazi mmoja wa Kike ambaye alifanikiwa kukimbia katika tukio hilo,huku maiti za Majambazi hao zikiwa zimehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maitiHospitali ya wilaya ya Kahama.

KWA PICHA ZA MAJAMBAZI WALIOUAWA TAZAMA HAPA CHINI.







VIONGOZI MBALIMBALI KATIKA PICHA



Mkuu wa Upelelezi wilayani Kahama George Bagyemu akionesha moja ya Risasi inayotumika katika Bunduki ya UZIGUN iliyokuwa ikitumiwa na Majmbazi

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ya Kahama ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo Vita Kawawa akizungumza na waandishi wa Habari wakati akilipongeza Jeshi la Polisi kwa kufanikiwa kuyauwa majambazi hayo na kukamata silaha zilizokuwa zikitumiwa na majambazi hayo

Mkuu wa Upelelezi wilayani Kahama George Bagyemu akionesha moja ya bomu la kurushwa kwa mkono lililokamatwa na Jeshi hilo kabla halijatumiwa na majambazi

Mbunge wa jimbo la Kahama Jumanne Kishimba wakati akizungumza kulipongeza Jeshi la Polisi kwa mapambano dhidi ya uhalifu wilayani Kahama.
SILAHA ZILIZOKAMATWA



No comments:

Post a Comment