Wednesday 27 April 2016

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA MAKATIBU TAWALA WAPYA WA MIKOA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha Makatibu Tawala wapya kumi aliowateua tarehe 25 Aprili, 2016 na kuwapangia vituo vyao vya kazi.

 Makatibu Tawala hao wameapishwa leo tarehe 27 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam na kisha wametia saini hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi lililoendeshwa na Kamishna wa maadili Sekreatieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mheshimiwa Jaji Salome Kaganda na kushuhudiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.

Makatibu Tawala walioapishwa ni;
  1.     Arusha -         Richard Kwitega
  2.     Geita -             Selestine Muhochi Gesimba
  3.     Kagera -          Armatus C. Msole
  4.     Kilimanjaro - Eng. Aisha Amour
  5.     Pwani        -    Zuberi Mhina Samataba
  6.     Shinyanga -    Albert Gabriel Msovela
  7.     Singida -         Dr. Angelina Mageni Lutambi
  8.     Simiyu -          Jumanne Abdallah Sagini
  9.     Tabora -         Dkt. Thea Medard Ntara
  10.     Tanga -           Eng. Zena Said
Makatibu Tawala wengine wa Mikoa ambao hawakuapishwa leo, ni wale waliohamishwa vituo vya kazi na wale waliobaki katika vituo vya kazi walivyokuwep,o ambao tayari walishakula kiapo cha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
27 Aprili, 2016

No comments:

Post a Comment