Wednesday 29 November 2017

WASAFIRISHAJI WA STENDI YA MABASI WALALAMIKIA UBOVU WA STENDI YA MKOA WA GEITA

DSC_0414
Muonekano wa stendi ya mabasi ya Mkoa wa Geita ikiwa imejaa maji kwenye baadhi ya maeneo.

DSC_0422

DSC_0430

DSC_0434

Wafanyakazi wa Stendi ya Mabasi makubwa Mkoani Geita wamelalamikia ubovu wa miundo mbinu ya stendi hiyo nakudai  kufanya kazi katika mazingira magumu kwa sababu ya wingi wa maji ndani ya stendi hiyo wakati wa mvua za masika.
Akizungumza kwaniaba ya wafanyakazi hao Khalid Hassani alisema matengenezo ya stendi hayakukidhi  vigezo  ndio sababu inayopelekea kuharibika mara kwa mara.

“Tumekua tukifanya kazi hapa stend lakini katika mazingira magumu kwasababu matengenezo ya stendi hayakukidhi haja wala vigezo hata matuta ya upande wakupaki magari yanayo ingia na kutoka hayapo na tumefikia hatua ya stendi kua na madibwi mengi kutokana na maandalizi kutokua mazuri’’ alisema Hassani.

Hassani alisema imekua ni aibu kwao wafanyakazi wa stendi hiyo kwa wageni wanao ingia na kutoka kutokana na hali ilivyo na Mkoa ambavyo umekuwa ukisifika kuwa na madini mengi ya dhahabu. 

Kwa upande wake mmoja wa wafanya biashara  Bi, Anipha Danieli alisema ndani ya stendi kuna maji mengi  hali inayosababisha kujaa kwa maji kwenye maeneo mengi.

“Mimi tangu tumeanza kuongea leo sio mara yangu ya kwanza tumechoka kuongea humu mwisho wake tutafuga samaki hii sio stendi jaman hata Geita napo tunatakiwa tuwe na stendi nzuri na iwe ya kisasa dhahabu zinatoka hapa lakini stendi yake sio tumeugua fangasi za miguuni kwaajili ya tope zilizomo humu’’ alisema Daniel

Kwa upande wake Mkurugenzi wa  halmashauri ya mji wa Geita,Mhandisi Modest Apolinary, alisema watu walitumia vibaya fedha za uma kutokana na kutokua na uaminifu na ameongeza kuwa wao kama halmashauri wanalitambua tatizo hilo na ameahidi kumwaga kokoto katika stend hiyo mapema wiki ijayo .

“kwa bahati mbaya hatukuwa na watu waaminifu watu walitumia fedha za uma vibaya ila uhalisia wa thamani  ya fedha  haikuonekana mwaka jana tulitumia zaidi ya milioni  ishirini na moja {21} mpaka million ishirini na tisa{29} kurekebisha na mwaka huu tena tunalijua hilo tumetenga million ishirini na moja{21} tunategemea kuanzia wiki kesho kufanya marekebisho” alisema Apolinary.



Apolinary alisema wanampango wa kutangaza tenda kwaajili ya kujenga stendi mpya Magogo ili  kutibu tatizo hilo nasio kumwaga pesa kila siku kwa ajili ya marekebisho  ya kila siku.

No comments:

Post a Comment