Friday 3 November 2017

BOT YAWAJENGEA UWEZO WA KUTAMBUA NOTI BANDIA WALEMAVU WA KUONA WILAYANI CHATO

Bw,Patrick Fata ambaye ni Mhelimishaji kutoka BOT akielekeza na kutoa elimu  namna ambavyo unaweza kutambua Noti bandia.

Meza kuu ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Chato Shaaban Ntarembe.

Maafisa wa BOT wakifuatilia maelezo ya Meneja Msaidizi wa Idara ya Uhusiano wa BOT, Vicky Msina wakati alipokuwa akielezea juu ya elimu ambayo wanaitoa kwa viziwi.

Meneja Msaidizi wa Idara ya Uhusiano wa BOT, Vicky Msina  akielezea malengo ya kutoa elimu ya kuwawezesha viziwi kutambua alama za usalama zilizopo kwenye noti ili kuzitofautisha na  noti bandia pindi wanapokuwa katika shughuli zao za utafutaji.

Mwenyekiti wa Kituo cha Sanaa na Utamaduni kwa Viziwi Tanzania (Kisuvita), Habibu Mrope akizungumza  changamoto ambazo wamekuwa wakikutana nazo watu ambao ni walemavu hususani wakati wanapokuwa wanakwenda kwenye huduma za kibenki.

Bw,Patrick Fata ambaye ni Mhelimishaji kutoka BOT,akisisitiza swala la alama za fedha ambazo zinakuwepo kwenye noti.

Kifaa ambacho kinatumika kuangalizia noti bandia na ile ambayo ni ya harari.

Noti ambazo zinakuwa zimeharibiwa zikiwa kwenye mafungu fungu lenye rangi nyekundi ni elfu kumi na yenye rangi ya blue ni elfu tano.

Benki  kuu ya  Tanzania (BOT)imekutana na  kundi la watu  wenye ulemavu wa kutokusikia na wale ambao hawaoni  Wilayani Chato lengo likiwa ni kuwapatia na elimu ya utambuzi wa Noti bandia Wilayani humo.
Akizungumza kwenye semina ambayo imefanyika kwenye ukumbi wa KKKT Wilayani Humo,Meneja msaidizi wa idara ya uhusiano wa BOT, Vicky Msina alisema elimu wanayoitoa imelenga kuwawezesha viziwi kutambua alama za usalama zilizopo katika noti ili kuzitofautisha na noti bandia wanapokuwa katika shughuli zao kwani mtu yeyote akikutwa na noti bandia ni kosa la jinai, hivyo wanawapa mafunzo ili wasikumbwe na kadhia hiyo.

“Ni muda sasa walituomba kuwapa mafunzo na hii ni kutokana na wengi wao kutokujua noti bandia wamekuwa wakijikuta wanabambikiwa na pia wanapo kwenda benki kupeleka fedha zao wahudumu huwadharau na wakati mwingine kwa wale wanao kwenda kuchukua fedha hupatiwa noti chafu jambo ambalo lilitusukuma kuwaelimisha juu ya hatua za kufuata ilikupatiwa haki zao za msingi kwenye huduma hizo,” Alisema Msima.

Mwenyekiti wa Kituo cha Sanaa na Utamaduni kwa Viziwi Tanzania (Kisuvita), Habibu Mrope alisema  kuna tatizo kubwa la kutotambua noti bandia kwa Walemavu hali ambayo imechangia kuwarudisha nyuma kwani wanapokutwa na noti hizo huchukuliwa hatua za kisheria.

Hata hivyo kutokana na tatizo hilo Mkuu wa wilaya ya Chato Shaaban Ntarambe aliwaahidi  watu ambao wanamatatizo ya kutokusikia kufunguliwa kwa shule ambayo itawasaidia kujifunza lugha za alama kwania ya kuboresha mawasiliano kwenye jamii.

“Idadi  ya wilaya yetu kuna  Viziwi 347 ambapo ni sawa na asilimia 90 ya watu wenye ulemavu wa kusikia hawajui lugha za nyakati  upekee idadi hii ni kubwa sana ni lazima Serikali ifanye jitihada za kuwa kwamua watu hawa ambapo kwa kushirikisha wadau mbali mbali, nitahakikisha ujenzi wa shule hiyo unaanza mara moja,” Alisisitiza Tarambe


Kwa upande wake mmoja wa washirki wa semina hiyo, Issa Pastori, mkazi wa Buziku wilayani humo alishukuru kupatiwa mafunzo hayo na kwa upande wa suala la uanzishwaji wa shule maalum ya lugha za alama ameomba mchakato huo uanze haraka kwani ni mkombozi kwao.

No comments:

Post a Comment