Friday 3 November 2017

NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT. NDUGULILE AIMWAGIA SIFA TFDA


 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Cheti cha Mfumo wa Uhakiki Ubora wa Huduma cha Kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) leo Jijini Dar es Salaam. TFDA imekuwa ya kwanza miongoni mwa mamlaka zinazoshughulika na udhibiti wa ubora wa chakula na dawa katika ukanda wa Afrika Masharika kutunikiwa cheti hicho.



Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Bw. Hiiti Sillo akielezea jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Cheti cha Mfumo wa Uhakiki Ubora wa Huduma cha Kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) leo Jijini Dar es Salaam. TFDA imekuwa ya kwanza miongoni mwa mamlaka zinazoshughulika na udhibiti wa ubora wa chakula na dawa katika ukanda wa Afrika Masharika kutunikiwa cheti hicho.



Mkurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Prof. Egid Mubofu akielezea jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Cheti cha Mfumo wa Uhakiki Ubora wa Huduma cha Kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) leo Jijini Dar es Salaam. TFDA imekuwa ya kwanza miongoni mwa mamlaka zinazoshughulika na udhibiti wa ubora wa chakula na dawa katika ukanda wa Afrika Masharika kutunikiwa cheti hicho.



Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Cheti cha Mfumo wa Uhakiki Ubora wa Huduma cha Kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) leo Jijini Dar es Salaam. TFDA imekuwa ya kwanza miongoni mwa mamlaka zinazoshughulika na udhibiti wa ubora wa chakula na dawa katika ukanda wa Afrika Masharika kutunikiwa cheti hicho. Kutoka kuhoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TFDA Dkt. Ben Moses, Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bw. Hiiti Sillo na Kaimu Meneja Uhakiki Mifumo wa TFDA Sunday Kisoma.



Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile wakiwa wameshika Cheti cha Mfumo wa Uhakiki Ubora wa Huduma cha Kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015) mara baada ya kuzinduliwa rasmi leo Jijini Dar es Salaam. TFDA imekuwa ya kwanza miongoni mwa mamlaka zinazoshughulika na udhibiti wa ubora wa chakula na dawa katika ukanda wa Afrika Masharika kutunikiwa cheti hicho. Kutoka kuhoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Prof. Egid Mubofu, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TFDA Dkt. Ben Moses, Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bw. Hiiti Sillo na Kaimu Meneja Uhakiki Mifumo wa TFDA Sunday Kisoma.


Naibu  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile ameipongeza Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) kuwa Mamlaka ya kwanza inayojishugulisha na udhibiti ubora wa chakula na dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki kutunukiwa Cheti cha Mfumo wa Uhakiki Ubora wa Huduma cha Kiwango cha Kimataifa (ISO 9001:2015).

Akzungumza katika uzinduzi wa Cheti hicho leo Jijini Dar es Salaam, Dkt  Ndugulile alisema cheti hicho cha ubora ni kielelezo cha Taasisi hiyo kusimamia misingi ya ubora katika utendaji kazi wake katika Mfumo wa uhakiki ubora wa huduma katika kiwango cha Kimataifa.

Ðk. Ndugulile amesema kuwa mafanikio hayo ya TFDA ni matokeo ya utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kuhakikisha huduma bora za afya hususani katika udhibiti na upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi.

“Utekelezaji wa mfumo huu na kupatikana kwa cheti hiki ni ishara nzuri kwamba TFDA inasimamia vyema mifumo yake ya kiutendaji ili kuhakikisha huduma zitolewazo zina ubora na zinakidhi matakwa ya kiwango cha Kimataifa cha ISO 900: 2015, hii pia inaleta imani kubwa kwa sisi tunaowasimamia utendaji wenu na wananchi wanaotumia bidhaa mnazozidhibiti kwa ujumla,” Alisema Dkt. Ndugulile.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo alisema mamlaka hiyo imetunukiwa cheti hicho kimeifanya taasisi hiyo kuwa Mamlaka ya kwanza miongoni mwa mamlaka zinazojihusisha na udhibiti wa ubora wa chakula na dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki na ya pili kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Aliongeza kuwa TFDA imekuwa ikitekeleza Mfumo wa Uhakiki Ubora wa Huduma kuanzia mwaka 2005 baada ya kufanya tathmini ya namna bora ya kufanya shughuli za udhibiti kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wateja.


“Katika kuendelea kukidhi matarajio ya wateja na kuendana na matakwa ya wateja wetu na wadau kwa ujumla, tuliamu kuboresha Mfumo wetu wa Uhakiki Ubora wa Huduma ili uendane na matakwa ya kiwango kipya cha Kimataifa, tulifanikiwa kutunukiwa cheti cha ISO 9001:2015 baada ya ukaguzi wa kina mnamo mwezi Agosti mwaka huu,” alisema Mkurugenzi Sillo.

No comments:

Post a Comment