Wednesday 8 November 2017

DC CHATO ATOA NENO KWA WAFANYABIASHARA JUU YA UUZAJI WA MBOLEA




Mkuu wa wilaya ya Chato mkoani Geita Mh. Shabani Ntarambe amesema hatawavulia wala kuwaonea aibu  baadhi ya wafanyabiashara watakao  uza mbolea kinyume na bei elekezi iliyopangwa na serikali.
Akizungumza na storm habari wilayani humo  mkuu huyo  amesema kuwa tayari wameshatoa elimu kwa viongozi wa vijiji na kata juu ya uuzwaji wa mbolea nakuwataka wafanyabiashara wa pembejeo za kilimo na mifugo kuhakikisha wanafuata bei elekezi iliyo tolewa na serikali ili kuwawezesha wakulima kulima kilimo chenye tija

Amesema atawachukulia hatua kali za haraka baadhi ya wafanyabishara  wanao haribu ubora wa mbolea nakuwa uzia wakulima makapi ya mbolea wilayani humo.


Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Buziku Bw. Magomamoto Zanzibar ameunga mkono jitihada za  mkuu wa wilaya nakusema kuwa  kwa mfanya biashara yoyote katika kata yake atakae bainika na tuhuma hiyo hata sita kumfikisha mahakamani

No comments:

Post a Comment