Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert
Luhumbi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita mhandisiModest
Apolinary kupeleka wakaguzi wa ndani wa Hesabu za Serikali Kata ya Mgusu ili wakakague
na kujiridhisha kuhusu mapato na matumizi ya Kata hiyo.
Akizungumza kwenye
ziara yake mjini Geita ya kuzindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na
zahanati Mhandisi Luhumbi amepokea malalamiko ya wakazi wa Machinjioni waliodai
kutosomewa taarifa za mapato na matumizi ya fedha zao.
Mhandisi Luhumbi
alisema kuwa endapo kama itakabainika kuwa kiongozi wa mtaa, kijiji au
Kata ametumia vibaya fedha za wananchi anapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria
na kuzirejesha fedha hizo.
“Mkurugenzi
leta timu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali ili ikague na kujiridhisha kama kuna
fedha yoyote iliyochukuliwa pasipo maelezo yanayojitosheleza hatua zichukuliwe
haraka kwa wote watakaobainika kuhusika". Alisisitiza
Luhumbi.
Mheshimiwa Robert
ameongeza kuwa ukaguzi huo ufanyike kuanzia mwaka 2014 hadi 2017 kisha apate
taarifa hiyo ofisini. Akiwa katika Halmashauri hiyo Mkuu wa Mkoa
amepongeza jitihada zinazofanywa na wananchi za kushiriki katika utekelezaji wa
miradi mbalimbali ya maendeleo licha ya kuwepo changamoto nyingi katika maeneo
yao.
Diwani wa Kata ya
Mgusu Bw Pastory Ruhusa amemueleza Mkuu wa Mkoa changamoto wanazokumbana nazo
kutokana na kukosekana kwa kituo cha afya kuwa ni pamoja na wakina mama
kujifungulia njiani na muda mwingine watu wengi wamejikuta wakipoteza maisha
kutokana na kukosekana kwa zahanati kwenye kata hiyo.
“Mkuu hapa
tumezungukwa na mgodi na ulituhaidi kutuchangia sh,milioni mia moj lakini
tunaona kama ni maneno tu kwani sasa imepita miaka miwili mgodi haujatekeleza
hiyo ahadi kiukweli tunapata shida sana kutokana na kwamba kata yetu ni mpya na
uhitaji ni mkubwa sanaa tunaomba msaada wako”Alisema Ruhusa.
Mkuu wa Mkoa
amehitimisha ziara yake ya Mkoa mzima katika Halmashauri ya Mji Geita kwa
kutembelea na kushirikiana na wananchi kujenga nyumba pacha ya walimu (Two in
one) Shule ya Msingi Shinamwendwa, ujenzi wa kituo cha Zahanati Mtaa wa Nyakato
, ujenzi wa vyumba vya madarasa viwili, ujenzi wa jengo la utawala shule ya
Sekondari Mgusu pamoja na kukagua eneo la kujenga Zahanati katika Kata
hiyo. Katika ziara hiyo ya Mkoa mzima Mheshimiwa Gabriel amefanikiwa
kutembelea Wilaya zote tano (5) na Halmashauri sita(6) na kufanikiwa kujenga,
kutembelea na kuanzisha jumla ya miradi 19 katika Sekta za Afya, Maji na Ujenzi
huku akikusanya zaidi ya mifuko 800 ya Saruji, tofali za Block 500, Mbao 50.
Haya yote ni matokeo ya kazi aliyoianza ya kushirikiana na wananchi kutekeleza
miradi ya maendeleo katika kila kijiji ndani ya Mkoa huu lengo kuu likiwa
kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo yao pia kupunguza
uhaba wa vyumba vya madarasa na Zahanati Mkoa humu.
Wananchi wote katika
maeneo aliyopita kufanya kazi wameonyesha kuridhishwa na utendaji kazi wa
Serikali na kuamua kuunga mkono juhudi hizi kwa kushiriki katika utekelezaji wa
miradi kama vile kusoma maji, kubeba mawe, mchanga, kokoto, kuchimba misingi na
vijana kujitolea kujenga miradi hii.
No comments:
Post a Comment