Monday 20 November 2017

SHIRIKA LA PLAN LIMETOA BAISKELI 191 ILI KUSAIDIA WATOTO MKOANI GEITA

DSC_0528
Baiskeli ambazo zimetolewa kwa wawakilishi wa kujitolea kwenye  jamii  na shirika lisilo la kiserikali la plan international mkoani Geita.

DSC_0534
Kushoto ni meneja wa Plan Mkoani Geita, Bw Marcel Madubi na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi  wakizungumza wakati wa zoezi la utoaji wa baiskeli.

DSC_0543
Meneja wa Plan Mkoani Geita, Bw Marcel Madubi akizungumzia malengo ambayo yamepelekea wao kutoa Baiskeli hizo kwa wawakilishi wa jamii.

DSC_0657
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akizungumza na wanufaika wa Baiskeli hizo.

DSC_0674
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akiendasha Baiskeli  ambazo zimekabidhiwa kwa wawakilishi wa jamii.

DSC_0687
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akimkabidhi Baiskeli Bi,Lucy John(Katikakati)pembeni kutoka kulia ni Mejena wa Plan ,Bw Marcel Madubi.

DSC_0699
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akimkabidhi Baiskeli,Mzee Geofray Kilomba na pembeni ambaye anapiga makofi ni,meneja wa plan Bw,Marcel Madubi.(PICHA NA JOEL MADUKA)

Shirika lisilo la kiserikali  la Plan International  ambalo linashugulikia masuala  ya kulinda na  kutetea haki za watoto hususani wa kike limekabidhi Baiskeli kwa wawakilishi wa kujitolea kwa jamii  kwaajiri  ya kurahisisha kuwafikia walengwa na  kutoa elimu dhidi ya ulinzi wa mtoto.

Akizungumza wakati wa zoezi la kutoa baiskeli  191 zenye gharama ya shilingi milioni 39,Meneja wa plan Mkoani Geita,Bw Marcel Madubi alisema kuwa  watoto wangi wamekuwa wakikumbwa  na  matatizo mengi likiwemo swala la mimba za utotoni na kuhozwa  mapema kitu ambacho kinaweza kukatisha ndoto zao za kimasomo.

“Wawakilishi wamekua ni kiungo kibwa kati yao na jamii katika kutafuta takwimu sahihi za watoto na kuwatafutia ufadhili na tangu plan ifike Geita kume kua na msaada wakuwatoa watoto kwenye utumikishwaji wa kazi zisizo sahihi  mfano kwenye maeneo ya migodi tumeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa” Alisema Madubi.

Kwa  upande wake Mkuu wa wilaya ya Geita Herman kapufi ambae alikua mgeni rasimi katika hafra hiyo alisema msingi wowote wa maendeleo unaanzia na mtoto kwahiyo ili Taifa liende  mbele nilazima watoto waangaliwe kwa umakini na kwamba chombo ambacho wamepatiwa wawakilishi kitawasaidia kwa kiasi kikubwa kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Bi,Scholastika Vitus ambaye ni mmoja kati ya wanafaika wa usafiri huo, alisema kunachangamoto nyingi zinawakumba watoto kama ukosefu wa mabweni hali ambayo inapelekea wengi wao kujikuta wakiingia kwenye mahusiano na waendesha boda boda ili mradi waweze kupata usafiri na kwamba endapo serikali itatilia maanani ujenzi wa mabweni itakuwa imemsaida mtoto wa kike kuepukana na vishawishi.

No comments:

Post a Comment