Thursday 23 November 2017

WANANCHI WILAYANI CHATO WAMEAHIDI KUSHIRIKIANA NA MKUU WA MKOA KATIKA KULETA MAENDELEO


Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akisisitiza wananchi kuendelea kujitokeza kwenye shughuli za maendeleo

Baadhi ya wananchi wilayani Chato mkoani Geita wameahidi kushirikiana na mkuu wa mkoa Mhandisi Robart Gabriel kwa kuwa ameonesha dhamira ya kuleta mabadiliko mkoani hapa.

Kauli hiyo wameitoa wakati wakifanya usafi katika eneo linalo tarajiwa kujengwa kituo cha afya cha kata ya mganza ambapo wamesema kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto

Kwa upande wake mganga mkuu wilayani humo Dakta Atanas Ngambakubi amebainisha kuwa wataanza na ujenzi wa jengo la huduma ya wagonjwa kisha kufatia nyumba za watumishi kwa lengo la kukifanya kituo hicho kuwa kinatoa huduma wakati wote.


Nae mkuu wa wilaya ya chato  Bw Shaban Ntarambe  amesema kuwa kufikia mwishoni mwa mwaka huu zoezi hilo litakuwa limekamilika.

No comments:

Post a Comment