Wednesday 8 November 2017

KILICHOENDELEA LEO MAHAKAMANI KUHUSU KESI YA HALIMA MDEE KUMTUSI RAIS MAGUFULI


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kuanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya kumtolea lugha ya matusi Rais John Magufuli inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee (39), December 7, 2017.
Wakili wa serikali, Leornad Challo amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa kesi imeitishwa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa lakini shahidi waliyenaye ana safari.

Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi December 7, 2017 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa.

Awali katika kesi hiyo Mdee aliposomewa maelezo ya awali inadaiwa July 3/2017 akiwa Makao Makuu ya Chadema, maeneo ya Ufipa alitoa lugha ya matusi dhidi ya Rais Magufuli.

Inadaiwa alitukana kuwa “Rais anaongea hovyo hovyo, inabidi afungwe break”.

Baada ya kutoa lugha hiyo, July 4/2017 alikamatwa na Polisi maeneo ya Kibangu, kisha kupelekwa kwa ZCO ambapo alihojiwa na kukiri kutoa maneno hayo.

Baada ya kusomewa maelezo hayo, Mdee alikubali wasifu wake ambao ni Jina, umri, nafasi ya uongozi, mahali anapokaa, kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Lakini alikana kumtolea lugha ya matusi Rais Magufuli, pamoja kukiri maneno hayo wakati akihojiwa katika ofisi za ZCO.

No comments:

Post a Comment