Monday 20 November 2017

WAKAZI WA WILAYA YA GEITA WAMEITIKIA VIZURI ZOEZI LA UANDISHAJI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA

DSC_0513
Wananchi wa Kata ya Buhalahala Mtaa wa Mwatulole wakiwa kwenye zoezi la kusajiliwa kwaajili ya kupatiwa vitambulisho vya Taifa.

DSC_0520
Baadhi ya watumishi wakiwa kwenye zoezi la uandikishaji wananchi vitambulisho vya Taifa.

DSC_0707
Mratibu wa NIDA Mkoani Geita,Bw Emmanuel Ernest akitoa elimu kwa wananchi juu ya zoezi la uandikishaji.

Wakazi laki moja na elfu kumi na mbili(112000)katika Halmashauri ya mji wa Geita wameandikishwa kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho vya taifa .

Zoezi la kuandikisha wananchi kwaajili ya kupatiwa vitambulisho vya Taifa limeanza mwezi August Mwaka huu na kwamba kwa mujibu wa sense ya mwaka 2012 ni watu Laki moja  na elfu themanini na saba wanatarajia kuandikishwa kwenye halmashauri hiyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mhandisi Modest Apolinary aliesema zoezi hilo limekuwa na mwitikio mzuri na wengi wanatamani kupata vitambulisho hivyo.

“Pamoja na changamoto ambazo zimejitoeza kwa baadhi ya wananchi lakini tunashukuru limekuwa na mwitikio mkubwa sana kwani watu wengi wamejitokeza kuandikishwa” Alisema Apolinary.

Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi alieleza kuwa  wamelenga kufikia mwezi Oktoba mwakani wawe wameandikisha wananchi wote kwenye halmashauri ya mji na ya Wilaya kufikia watu elfu tano.

Bw Joseph Bwire ambaye ni mkazi wa Mtaa wa mkoani na Bi Magdalena Manyirizu  walisema vitambulisho hivyo vitawasaidia kutambulika  na pia kupata mikopo kwenye mashirika ya kifedha.
Afisa usajili wa NIDA Mkoa wa Geita Bw Emmanuel Ernest alisema  wanatarajia kwenye Mkoa mzima kusajili wananchi milioni moja wenye sifa ndani ya Mkoa huo.

No comments:

Post a Comment