Tuesday 14 November 2017

WACHIMBAJI WADOGO NYARUGUSU WAJITOLEA KUJENGA MADARASA

DSC_0351

 Madarasa ya shule ya msingi ya  Tologo ambayo yamejengwa na wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu. 

DSC_0296

Evarist Pascal  ambaye ni mchimbaji mdogo akitoa maelezo kwa mkuu wa Wilayaya Geita(ambaye yupo katikati)shughuli za ujenzi na ghalama ambazo zimetumika kujenga madarasa hayo. 

DSC_0299

 Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akishukuru kwa kazi ambayo imefanywa na wachimbaji wadogo wa kata ya Nyarugusu Wilayani humo. 

DSC_0312

 Madarasa ya shule ya msingi ya  Tologo ambayo yamejengwa na wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu. 

DSC_0341

 Diwani wa Kata ya Nyarugusu,Swalehe Juma akielezea na kuonesha darasa ambalo bado halijakamilika. 

DSC_0380


 Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl,Herman Kapufi pamoja na viongozi wa kijiji na kata na wachimbaji wakitoka kwenye eneo la shule.


Wachimbaji wadogo kwenye Kata ya Nyarugusu na Serikali ya kijjiji na kata  hiyo wameshirikiana kuchangia ujenzi wa madarasa manne na ofisi 2 za walimu kwenye Shule ya Msingi Tologo iliyoezuliwa na upepo na kubaki darasa moja.

Akizungumza na mkuu wa wilaya ya Geita , wakati alipokwenda kujionea shughuli na jitihada ambazo zinafanywa na wachimbaji wadogo za kuboresha miundo mbinu ya elimu,Bw Evarist Pascal alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa hali ambayo ilisababisha wanafunzi kusomea madarasa ambayo yalikuwa yameezuliwa na mvua walionelea ni vyema wakichangia ujenzi huo hili  watoto wapate sehemu nzuri ya kujisomea.

Hata hivyo ameendelea kutaja kuwa ujenzi wa madarasa hayo pamoja na ofisi za walimu umegharimu kiasi cha  Sh, Milioni 56.

Aidha ameendelea kusema kuwa  kitongoji cha Tologo kinakabiliwa na upungufu wa zahanati ya mama na mtoto kwa kuwa ipo zahanati moja ya Boko ambayo imeelemewa na kwamba ili kuchangia ujenzi huo wametengeneza madirisha 11 na kufyatua matofali elfu 3

Kutokana na juhudi ambazo wamezifanya Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi amewapongeza wachimbaji hao na ameahidi kushirikiana nao ili kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo .

No comments:

Post a Comment