Friday 10 November 2017

SERIKALI WILAYANI CHATO KUTAIFISHA VYOMBO VYA MOTO VITAKAVYO SAFIRISHA SAMAKI WADOGO



Serikali wilayani Chato  mkoani Geita imeahidi kuvitaifisha vyombo vyote vya moto vitakavyokamatwa vikisafirisha samaki wachanga kutoka ziwa victoria  kwenda maeneo mengine ndani na nje ya wilaya hiyo.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Chato  Shabani Ntarambe wakati  akizungumza na storm habari  ofisini kwake juu ya uvuvi haramu mbapo amesema kuwa wamejipanga kuhakikisha wanakagua magari na pikipiki kwa lengo la kuwabaini baadhi ya watu wanaosafirisha samaki wachanga kinyume na sheria.

Amesema hatua hiyo imekuja mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema juu ya uwepo wa madereva bodaboda  na magari ya abiria wanaotumia vyombo hivyo kutorosha samaki wachanga jambo ambalo halikubariki.

Aidha  mwenyekiti wa uhifadhi wa rasilimali za uvuvi BMU  wilayani humo Bw Bashiri Manampa amesema  kuwa amejipanga kuanzisha msako mkali kwa kushirikiana na maofisa wa uvuvi wilayani humo kwa lengo la kuendelea kupambana na wavuvi haramu katika ziwa victoria.

No comments:

Post a Comment