Wednesday 15 November 2017

GEITA WAZINDUA RASMI MSIMU WA KILIMO CHA PAMBA MWAKA 2017

DSC_0537
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akishiriki zoezi la upandaji wa mbegu za pamba kwenye shamba la watumishi wa halmashauri ya mji wa Geita.
DSC_0512
Mkuu wa Mkoa wa Geita,akiwasili kwenye eneo la shamba na kusalimiana na viongozi wa halmashauri hiyo akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi.


DSC_0517
Afisa Kilimo wa halmashauri ya mji,Bw Samwel Ng'wandu akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita pamoja na mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Geita,Leornad Kiganga.

DSC_0550
Baadhi ya watumishi na Jeshi la akiba (MGAMBO)wakishiriki shughuli za kupanda mbegu kwenye shamba la watumishi wa halmashauri ya mji.

Wataalamu wa kilimo mkoani Geita wametakiwa  kuwafuatilia kwa karibu wakulima wa pamba na kuwaelekeza kulima kwa tija ili kuzalisha zaidi tofauti na miaka ya nyuma.

Akizindua msimu wa kilimo cha pamba kwenye mashamba ya watumishi wa Halmashauri ya mji wa Geita yaliyoko kata ya Buhalahala ,Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi alisema  ni vema wataalam hao wakafika kwenye maeneo ya kilimo na kuwaelekeza wakulima kanuni zitakazowasaidia kuvuna pamba nyingi.

“Wito wangu kwa wakulima wote pamoja na wataalam wetu wa kilimo baada ya uzinduzi huu mkubwa kabisa wa kilimo cha pamba Mkoani  kwetu,wataalam ni vyema wakawasaidia  wakulima kufuata zile kanuni  kumi bora za kilimo ambacho kitaweza kuwa saidia wakulima lakini nataka twende kisayansi zaidi” Alisema Luhumbi.

Mhandisi Luhumbi Aliongezea Kuwa  Serikali ya awamu ya tano  imedhamiria kumsaidia mkulima na kuwataka wakulima kuchangamkia fursa hiyo na kuwekeza katika sekta ya kilimo cha pamba kwa kuwa hali ya hewa ya mwaka huu ni nzuri.

Mshahuri wa kilimo cha Mkataba Mkoani Geita Bw Joshua Mirumbe alisema lengo ni kuhakikisha wanaongeza tija ya uzalishaji kutoka wastani wa kilo 250 hadi 300 na kwenda kwa wastani wa kilo 800.


Katika msimu wa mwaka 2016/2017 mkoa wa Geita ulilenga kulima hekta 67002  zilizotarajiwa kuzalisha tani ,93437 za pamba lakini utekelezaji ulikuwa hekta  24 791 zilizozalisha tani  13 267.8 zenye thamani ya Sh Bilioni 15.

No comments:

Post a Comment