Friday 10 November 2017

WAHITIMU WA MGAMBO GEITA WAOMBA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWENYE MAKAMPUNI

DSC_0430

 Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl,Herman Kapufi  akiongozana na kiongozi Mkuu wa Gwaride pamoja na Mshauri wa majeshi ya akiba Wilayani humo,Luteni Kanali ,Daud Issah Mnyanga wakati walipokuwa wakikagua gwaride. 

DSC_0410

 Mkuu wa wilaya ya Geita  Mwl,Herman Kapufi ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Wilayani ,Humo akiimba wimbo wa Taifa mala baada ya kuwasili kwenye viwanja hivyo. 

DSC_0413

 Baadhi ya viongozi wa serikali pamoja na kamati ya ulinzi na usalama wilayani humo wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa zoezi la kufunga mafunzo ya  jeshi la akiba(Mgambo).
 
DSC_0454

  Baadhi ya askari wa jeshi la akiba wakijiandaa kupita mbele ya mgeni rasmi kwaajili ya kutoa heshima. 

DSC_0456

 Moja kati ya viongozi wa Gwaride akiongoza askari wa Mgambo wakati walipokuwa wakitoa heshima kwa mwendo wa taratibu mbele ya mgeni rasmi. 

DSC_0470

 Mkuu wa Wilaya ya Geita akitazama shughuli na burudani ambazo zilikuwa zikifanyika wakati wa zoezi hilo. 

DSC_0471

 Gwaride likipata kwa mwendo wa taratibu mbele ya mgeni rasmi. 

DSC_0479


 Mkuu wa Wilaya ya Geita pamoja na viongozi wengine wakiwa wamesimama wakati Gweride lilipokuwa likipita mbele kwaajili ya kutoa heshima. 


DSC_0512 

DSC_0519

 Makomandoo wa jeshi la akiba wakionesha namna ambavyo wamehiva kwenye suala la kupamba na adui. 


DSC_0530

 Baadhi ya wananchi wakifuatilia maonesho ambayo yalikuwa yanafanywa na jeshi la akiba. 

DSC_0537

DSC_0540

DSC_0543




DSC_0598

 Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwk Herman Kapufi akiwatunuku vyeti baadhi ya askari wa mgambo ambao wamehitimu mafunzo. 

DSC_0615

 Mshauri wa jeshi la akiba  wilayani Geita Luteni Kanali ,Daud Issah Mnyanga akimkaribisha mgeni rasmi wakati wa shughuli za kuwaaga askari wa jeshi la akiba. 

DSC_0655

 Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akiwahutubia baadhi ya askari ambao wamefudhu mafunzo hayo.




Vijana waliohitimu mafunzo ya jeshi la akiba ama Mgambo wilaya Geita, wameiomba serikali kuwapa kipaumbele katika fursa za ajira za ulinzi zinazojitokeza na pia mikataba ya walinzi izingatie maslahi yao.

Akisoma Risala kwa mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi, Muhitimu wa mafunzo hayo Helena Nyamtondo alisema ni vyema kwa serikali ikatoa fursa za ajira kwenye Nyanja mbalimbali kwa wahitimu wa mafunzo hayo yakiwemo makampuni binafsi ya ulinzi ambayo yapo wilayani humo.

“Ndugu Mgeni rasmi tunaomba kupitia mafunzo haya sisi kama wahitimu tupate nafasi kwenye makampuni ya ulinzi yakiwemo ya G4S na Mgodini kwakuwa tunaweza kutumia kile ambacho tumefundishwa kuweka usalama kwenye maeneo hayo na swala jingine ni mishahara na mikataba ya walinzi kutokuwa na masirahi hivyo tunaomba kuboreshewa masirahi ya kazi zetu” Alisema Bi,Nyamtondo.

Mkuu wa wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi alisema  katika kuhakikisha kuwa anashughulikia maombi yao wiki ijayo atakutana na viongozi wa makampuni ya ulinzi kuzungumza nao kuona namna wanavyoweza kuwasaidia wahitimu wa mafunzo hayo kupata ajira kwenye mashirika yao.

Kwa upande wake mshauri wa Mgambo wilayani Geita Luteni Kanali Daud Mnyanga alisemaa katika mafunzo ya mwaka huu wamekutana na changamoto ya vijana kutofika kwa wakati na tatizo la kifedha .


Jumla ya wahitimu 195 wametunukiwa vyeti vya kuhitimu mafunzo hayo huku 28 wakishindwa kuhitimu kati ya washiriki 223 walioanza mafunzo hayo awali.
 

No comments:

Post a Comment