Wednesday 16 March 2016

WAZIRI MKUU AWAAGIZA WAKUU WA WILAYA KUHAKIKISHA WATOTO WOTE WANAKWENDA SHULE.


Waziri mkuu  wa jamuhuri ya muungano wa  Tanzania Mh.kassim majaliwa amewaagiza wakuu  wa wilaya nchini kuhakikisha kuwa   wanawafatilia watoto  wote  ambao   walifaulu kujiunga na  masomo ya sekondari kuhakikisha wanakwenda shule.


Ametoa agizo hilo wakati alipokuwa akipokea taarifa ya mkoa wa geita juu ya utekelezaji wake wa maendeleo amesema wakuu wa wilaya wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanasimamia kila mtoto ambaye amefaulu anakwenda kuanza masomo ya sekondari na kuachana na swala la utoro na kwamba kwa sasa wazazi hawana sababu ya kuwazuia watoto kusoma kwani  elimu  ni bure.

Aidha  waziri Majaliwa ameongeza kuwa ni vyema kuhakikisha kuwa wale wote ambao wamewasababishia watoto wa kike kutokuendelea kupata elimu kuwachukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwasaka na kuwafikisha katika ngazi ya sheria.

Akiwakilisha wakuu wa wilaya ,mkuu wa wilaya ya Nyang’wale Mh.Ibrahimu Malwa,amesema kuwa agizo la waziri mkuu wamelipokea na kwamba watahakikisha kuwa wanatekeleza kile ambacho kimeagizwa  kwa kuhakikisha wanawafatilia watoto ambao wanajihusisha na maswala ya uchimbaji ili waweze kwenda shule na kwamba wale wote ambao wamekuwa wakifanya tabia za kuwaajiri watoto watahakikisha wanachukuliwa hatua za kisheria.


Waziri mkuu Mh.Kassim Majaliwa yupo mkoani hapa kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo leo ameweza kupokea taarifa ya mkoa na kuzindua duka la dawa la (MSD) katika hospitali ya wilaya ya Chato na pia kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara wilayani hapo.

No comments:

Post a Comment