Wednesday 23 March 2016

WATOTO WAWILI WA FAMILIA MOJA WAPOTEZA MAISHA BAADA YA KUZAMA KWENYE DIMBWI LA MAJI MKOANI GEITA.


Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Geita, Lotson Mponjoli


Watoto wawili wa familia moja wamefariki dunia  baada ya kuzama kwenye  dimbwi la maji  lililopo mtaa wa elimu,kata ya Nyankumbu mkoani Geita.

Akithibitisha kutokea kwa tukio  hilo kamanda wa polisi mkoa wa geita Mponjoli Mwabulambo amesema waliofaliki ni Ladislaus  mwenye umri wa miaka kumi mwanafunzi wa darasa la 4  katika shule ya msingi Mseto  pamoja na Adela Jonas mwenye umri wa miaka  3.

Kamanda Mponjoli amesema kuwa baada ya jeshi la polisi kufika katika eneo la tukio walikuta ndoano na samaki wamevuliwa kwenye maji kitendo ambacho kinaonyesha kuwa watoto hao walikuwa wanavua samaki.

Hata hivyo storm fm  ilimtafuta mwenyekiti wa mtaa huo Hassan Mushora ambapo baada ya kufanikiwa kufanya nae mazungumzo alisema kuwa taarifa za tukio hilo kama mwenyekiti alilipata majira ya saa 9 alasiri tayari watoto hao wakiwa wamepoteza uhai.

Akizungumza na storm habari baba mwenye nyumba Bw. Paulo Masanja ambapo watoto hao walikuwa wakiishi na mlezi wao wa kike ambaye hakufahamika jina kwa haraka   amesema siku ya tukio mama huyo aliwatuma watoto wakachote maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani .


Mmoja wa shuhuda nyumbani hapo   Lucia Paulo alisema siku hiyo watoto  watatu walienda kufuata maji  mmoja  wa watoto hao alirudi na kumwambia mama yake  wenzake wamezama ndani ya dibwi  ndipo mama huyo aliamua kwenda kuwaangalia na kuwakuta  wamepoteza maisha

No comments:

Post a Comment