Saturday 12 March 2016

MACHIMBO YA MGUSU MKOANI GEITA YASIMAMISHWA KWA MUDA.


Mkuu wa mkoa Geita Bi.Fatuma Mwasa(kushoto)na Naibu waziri wa nishati na madini Dkt.Medard Kalemani(mwenye suti nyeusi).
Serikali imewataka Wachimbaji wa Eneo la Mgusu kutoingia eneo la uchimbaji hadi pale itakapofanyika marekebisho ya ulipuaji wa mwamba uliobaki katika shimo lilosababisha kufukiwa kwa baadhi wachimbaji ambapo watano walifariki na watatu kujeruhiwa.


Matukio ya kufukiwa kwa wachimbaji wadogo yamekuwa yakijitokeza mara kadhaa ambapo takwimu zinaonyesha kuanzia mwaka 2010 hadi 2016 matukio yaliyoripotiwa ni 34 na yalisababisha vifo vya watu 49.

No comments:

Post a Comment