Friday 25 March 2016

ULINZI KUIMARISHWA MKOANI GEITA KWENYE SIKUKUU HII YA PASAKA.


Kamishina msaidizi wa jeshi la polisi mkoani Geita, Mponjoli Lotson.

Jeshi la polisi mkoani Geita  limejipanga kuimarisha ulinzi  na usalama katika sikukuu ya pasaka itakayoadhimishwa jumapili march  27 duniani kote  ili kuwawezesha wananchi kusherehekea kwa amani na utulivu siku hiyo.


Akizungumza na storm habari ofisini kwakwe kamishina msaidizi wa jeshi la polisi mkoani hapa, Mponjoli Lotson  amesema kuwa uamuzi huo umekuja baada ya kugundua kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakitumia mwanya huo kufanya uhalifu kutokana na kuwepo kwa muingiliano mkubwa wa wananchi katika sehemu mbalimbali.

Aidha kamanda Mponjoli amebainisha kuwa  maeneo yote  wameimarisha ulinzi ikiwemo kumbi za starehe, makanisa, sehemu zote za njia kuu, huku  askari wakipangwa kila mitaa.


Aidha kamanda amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kutoa taarifa sehemu husika pindi wanapokuwa na  na mtu ama kikundi cha watu.

No comments:

Post a Comment