Tuesday 15 March 2016

WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA WILAYANI MBOGWE,MKOANI GEITA WAILALAMIKIA SERIKALI.



Wakulima wa zao la pamba katika kata ya Ikunguigazi wilayani Mbogwe mkoani Geita wameilalamikia serikali kwa kuwaingiza kwenye kilimo cha mkataba ambacho wamekuwa wakikabiliwa na hujuma nyingi zikiwepo kuuziwa mbegu feki, bei kuwa chini mizani iliyochakachuliwa na sasa wamesambaziwa dawa za viuatirifu feki ambazo haziui wadudu.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti na storm habari wamesema kuwa dawa walizosambaziwa na umwapa haziuwi wadudu  hali ambayo imeendelea kupelekea zao la pamba kuendelea kuharibika kutokana na kuliwa na wadudu.

Diwani kata ya Ikunguigazi Lutandula Kazimoto ameiomba Serikali kuhakikisha inakuja kuchunguza kila shamba na ikiwezekana iwasaidie wakulima wa zao hilo kuwapatia fidia ya sehemu ambazo zimeharibika kutokana na dawa hizo.


 Kaimu Afisa kilimo wilaya ya Mbogwe Stephen Shilemba amesema kuwa  tatizo  kubwa la wakulima wanashindwa kufuata maelekezo na masharti ya uchanganywaji wa dawa wanataka dawa kidogo ipulizie heka nyingi ili kubana matumizi hivyo shida iliyopo kwa wakulima ni elimu, bado hawajaelewa wanatumia mazoea  hivyo amewataka kuacha  mazoea na ni vyema  wakafuata masharti ya kitaalamu.

No comments:

Post a Comment