Mwanasheria wa shirika lisilo la kiserikali la Woman Promotion Center ,Bi, Walta Caros akizungumza na waandishi wa habari juu ya sheria ya vitendo vya kikatili kwa mwanamke.
Hofu na kutojiamini ni miongoni mwa sababu za wanawake wengi wanaofanyiwa
ukatili kushindwa kutoa taarifa na kujikuta wakipoteza haki zao ikiwemo
kudhurumia baadhi ya mirathi pindi waume zao wanapofariki.
Hayo yamebainishwa
katika kikao cha Shirika lisilo la kiserikali la Woman Promotion Centre na
maafisa ustawi wa jamii, watendaji wa mitaa na kata pamoja na Madiwani wa
halmashauri za mkoa wa Geita ili kujadili mapungufu ya sera na sheria za nchi
zinazohusu masuala ya kijinsia na haki za wanawake.
Afisa maendeleo ya
jamii wa Halmashauri ya mji wa Geita Bi Mariam John amesema wanawake wengi
wanahofia pale wanapoambiwa kesi zipelekwe mahakamani hali inayosababisha wengi
wao kuendelea kunyanyasika .
“Tatizo kubwa ambalo
limeendelea kuwakuta wanawake wengi ni kuendelea kuwa wasili kwa maana ya
kutokutoa taarifa ambazo zitasaidia kufikishwa kwenye ngazi za kisheria na hata
tunapotaka kufikisha kwenye ngazi hizo wengine wamekuwa wakiogopa” Alisema Mariam.
Mwanasheria wa Shirika
hilo Bi Walta Carlos amesema kuna umuhimu wa kuwepo kwa sheria au sera
itakayozungumzia ukatili kwa wanawake kwa kuwa kumeendelea kuwepo kesi nyingi
za ukatili.
“Nadhini ni wakati
umefika kwa serikali kuona umuhimu wa kuwepo kwa sera au sheria ambayo
itasimamia na kuzungumzia kwa marefu na mapana suala la wanawake na wasichana
ambao wameendelea kufanyiwa ukatili hii ni kutokana na sheria iliyopo kwa sasa
kuwa na mapungufu mengi” Alisema Mwanasheria Walta.
|
No comments:
Post a Comment