Tuesday 29 March 2016

RAIS MAGUFULI AZITAKA KAMATI ZA SHULE MKOANI GEITA KUSIMAMIA NIDHAMU NA UTORO SHULENI

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr, John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wilayani Chato mkoani Geita
Rais  wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr,John Pombe Magufuli amezitaka kamati zote za shule kuhakikisha kuwa zinasimamia swala la nidhamu na utoro katika shule  wanazoziongoza  na kama kuna kamati yoyote ambayo itashindwa ni vyema ikajihuzuru mapema.


Wito huo ameutoa mapema leo wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Chato mkoani Geita,katika shule  ya sekondari Chato,ambapo amesema kuwa kwa kamati yoyote ambayo  itashindwa kuhakikisha kuwa inadhibiti suala la nidhamu mashuleni ni vyema ikajiondoa mapema.

Rais Magufuli amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii na wazazi kuhakikisha kuwa wanawafatilia  watoto pindi wawapo  shuleni ili kuweza  kutengeneza Tanzania  ya wasomi zaidi.

Aidha wananchi  wilayani humo,wamemshukuru Rais Magufuli kwa ujio wake huku pia  wakimpongeza kwa uchapakazi wake uliotukuka na kwamba wamemwomba kuendelea kuwaondoa watumishi wote ambao hawana maadili ya kazi.


Rais,Magufuli amewataka watanzania kuendelea kupendana  na kuwa wamoja na kuachana na fujo  na malumbano ambayo yanaweza kupelekea kutowesha amani ya nchi.

No comments:

Post a Comment