Friday 11 March 2016

MRATIBU WA TASAF WILAYANI MBOGWE MKOANI GEITA AMEWAONYA WATENDAJI WANAOHARIBU MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI.


Mratibu wa TASAF wilayani Mbogwe mkoani Geita Bi.Mercy Joseph Kabaka amewaonya baadhi ya wenyeviti na watendaji vijiji walioharibu zoezi kwa kuingiza walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini wasiokuwa na sifa hizo na kuwataka wahakikishe wanaitisha mikutano mikuu ya vijiji ili kuwaondoa mara moja.


Bi.Kabaka amesema kuwa kumejitokeza malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi toka vijijini wakilalamika kuwa kuna watu wanafaidika na mpango lakini si maskini kwani walipitisha kimakosa kwa kuangaliwa kuwa ni ndugu, ukoo, chama ama dini fulani.

Mratibu huyo amewaonya  wanyeviti wa vijiji  kuwa wao ni wanasiasa lakini TASAF si ya kisiasa wala udini ama ukabila lengo lake kubwa ni kuwasaidia watanzania  wanatoka kaya maskini ili waweze kuinuka kiuchumi  lakini  imebainika wao wameipotosha TASAF kwani wameingiza kaya ambazo si maskini hivyo wahakikishe wanazibaini kaya hizo na kuziondoa haraka.

Kabaka ameongeza  kuwa agizo la waziri Kairuki wamelipokea na pia amethibitisha kuwa hali hiyo ya kuingizwa kwenye mpango wasiokuwa na sifa kwa baadhi ya vijiji hali hiyo ipo,kwani tayari katika ofisi yake wamekwisha pokea malalamiko toka kwa wanajamii kuwa wao ni kaya maskini lakini majina yao yaliachwa kwa vile wenyeviti na watendaji waliangalia vyama, ukoo,udini hivyo na wao wanaomba waingizwe kwenye mpango huo.


Wilaya ya Mbogwe ina jumla ya vijiji 60 ,kaya zipatazo elfu 4,834  na kiasi cha zaidi ya sh milioni mia moja tisini na tisa, laki tisa  arobaini  na saba elfu na sitini na nane (199,947,068.18 ) zinagawiwa katika vijiji hivyo.

No comments:

Post a Comment