Friday 9 March 2018

RC LUHUMBI :VYOMBO VYA HABARI VISHIRIKI KUFICHUA UOVU DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

Mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi ambaye alikuwa ni mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake ambayo  kimkoa yamefanyikia Wilayani Bukombe.akiwahutubia wananchi ambao walikuwa kwenye viwanja vya stendi ya mabasi ya ushirombo.
Maandamano ya wanawake wakielekea katika dhifa ya maadhimisho ya siku ya wanawake ambayo katika Mkoa wa Geita yamefanyika Wilayani Bukombe.

Baadhi ya wakina mama wakionesha mabango ambayo walikuwa wamebeba wakati wa maandamano mbele ya mgeni Rasmi.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko ambaye pia ni Naibu Waziri Wa Madini akizungumza  wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake ambayo katika Mkoa wa Geita yamefanyika Wilayani Bukombe.

Mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi ambaye alikuwa ni mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake,akikagua baadhi ya bidhaa ambazo zimetengenezwa na wakina mama wajasiriamali.






Ni miaka 73 tangu Umoja wa Mataifa (UN), kupitisha maazimio ya tarehe ya leo kila mwaka kuwa siku ya maadhimisho ya siku ya wanawake kwa lengo la kupaza sauti zao juu ya ukandamizaji na ukatili ambao umewafanya washindwe kushiriki maendeleo endelevu ya familia na taifa kwa ujumla.

Chimbuko la Siku ya Wanawake Duniani lilianza miaka mingi na mwaka 1911, baada ya Wanawake nchini Marekani kuandamana kudai haki zao ambazo walikuwa wakizikosa: kama vile kulipwa ujira mdogo, kufanyishwa kazi ngumu na kwa masaa mengi, kukosekana kwa huduma za jamii na ubaguzi wa kijinsia.

Kila mwaka maadhimisho haya yanafanyika na kubainisha changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake na kuwa kikwazo kikubwa cha kusonga mbele katika kujikwamua kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa.

Mkoani Geita maadhimisho haya yamefanyika wilayani Bukombe,huku yakiuzuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali akiwemo Mkuu wa mkoa huo Mhandisi , Robert Luhumbi pamoja na Naibu waziri wa madini ambaye pia ni mbunge wa Jimbo hilo Doto Biteko.

Mkuu wa mkoa huo ambaye alikuwa ni mgeni rasimi ametumia nafasi hiyo  kuvitaka vyombo vya habari kuendelea kuibua na kutangaza vitendo vya ukatili  ambavyo vimekuwa vikifanywa dhidi ya wanawake  na watoto ndani ya jamii.

Vyombo vya habari wakiwa ndio wadau wakuu wa kuibua masuala mbali mbali yasiyo ya haki ndani ya jamii ,kwa kushirikiana na serikali na jamii yote ,ushirikiano wenu wa dhati wa kusaidia kuibua vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto ndani ya jamii,una umuhimu mkubwa .Pia niwasihi Jeshi la polisi ,kuimarisha madawati ya jisnia na watoto kwenye vituo vya Polisi na kushirikiana kikamilifu na wadau wa harakati za kuwakomboa wanawake na watoto kwa ajili ya kusaidia kupokea ,kufuatilia na kushughulikia kesi za ukatili na unyanyasaji wa kijinsia kwa uharaka zaidi” Alisema Luhumbi.

Akisoma Risala  mbele ya mgeni rasmi Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake Wilayani humo,Bi Leticia Mourice alisema maendeleo ya wanawake katika Nyanja mbali mbali hapa nchini ,yamekuwa yakikwamishwa na nafasi ambazo wanazo wanawake kama wazazi walezi na wafanyakazi.

“Kwa upande mwingine ,mila na desturi kandamizi kwa baadhi ya maeneo ,zimeendelea kujengwa na kukuzwa.Jambo hili limeleteleza kutokuwepo na usawa kwa Jinsia katika Sekta zote za maendeleo hususani katika Nyanja ya elimu,ajira,afya,umiliki wa rasilimali ardhi,urithi na ushirikishwaji katika ngazi mbali mbali za maamuzi” Alisema Bi. Leticia,


Siku ya wanawake Duniani imepambwa na kauli mbiu isemayo” Kuelekea uchumi wa viwanda, tuimalishe  usawa wa jinsia na uwezeshaji wa wanawake vijijini"


No comments:

Post a Comment