Thursday 8 March 2018

UHABA WA MADARASA WASABABISHA WANAFUNZI KUSOMEA NJE GEITA.

Wanafunzi wa shule ya msingi Mchongomani iliyopo kata ya Katoro Wilayani Geita wakisoma nje kutokana na uhaba wa madarasa.

Wanafunzi wa shule ya msingi Mchongomani wakiwa nje wakati wa masomo kutokana na uhaba wa madarasa.

Choo cha wanafunzi ambacho kinamatundu matatu na kinatumiwa na wanafunzi 2072 shuleni hapo.

Wanafunzi wa shule ya msingi Mchongomani kata ya Katoro mkaoni Geita  wanasomea nje wakiwa wamekaa chini na wengine kubanana kwenye madawati  kutokana na shule hiyo kukabiliwa na Upungufu wa madawati na vyumba vya madarasa.


Baadhi ya wanafunzi hao Jesca Michael na Hoja Hassan wamesema hali  hiyo imekuwa ikisababisha utoro kwa baadhi ya wanafunzi na kwamba mvua zinaponyesha wamekuwa wakisitisha masomo.

“Tumekuwa tukipata shida kubwa sanaa kusomea nje hali hii imekuwa ikisababisha baadhi ya wanafunzi wenzetu kushindwa kuja shule kutokana na haya mazingira ya kusomea nje” Alisema Jesca.

Tunaathirika sanaa macho kusomea nje kwani muda mwingine jua likiwa kali limekuwa likituumiza macho na siku nyingine mvua zikinyesha uwa tunashindwa kusoma hali hii imekuwa ikisababisha kushindwa kufanya vizuri kwenye masomo yetu tunaomba serikali itusaidie kwani tunateseka sanaa hadi muda mwingine tunawaonea huruma walimu wetu." Alisema Hoja.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw Faustine Makulu  amekili kuwepo kwa tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa na kwamba uhitaji wa vyumba vya madarasa ni 46 na kwasasa wamejenga vyumba 4 na vinavyotumika ni viwili huku wanafunzi waliopo shuleni hapo ni 2072.

“Hapa shuleni kwangu hali siyo nzuri pamoja na jithada ambazo zimeendelea kufanywa na serikali lakini uhitaji ni mkubwa sanaa ukilinganisha na watoto waliopo na madarasa ambayo yapo utaona hali ilivyo kiuweli hadi sasa hivi jitihada ambazo zinaendelea ni ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa”Alisema Mwalimu Makulu.

Aidha Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Geita, Bw Ali Kidwaka alisema  wanafanya jitihada za kujenga vyumba vya madarasa 322 wilayani humo vikiwemo katika shule hiyo na kwamba wanatarajia kufikia Desemba mwaka huu wawe wamepunguza changamoto ya upungufu wa madarasa.

No comments:

Post a Comment