Thursday 29 March 2018

BAADHI YA MAKAZI WILAYANI CHATO YAHARIBIWA NA MVUA








Zaidi ya kaya 139 katika kijiji cha mkuyuni kata ya chato wilayani chato mkoani Geita zimekumbwa na mafuriko ya maji kufuatia mvua zinazo endelea kunyesha huku kaya 24 kati ya hizo zikikosa mahala pakuishi baada ya nyumba zao kubomoka.


Baadhi ya wahanga wa tukio hilo wameimbia storm habari kuwa kadhia hiyo imetokana na mvua kubwa iliyo nyesha March 26 mwaka huu nakusababisha maji kuzingira na kujaa ndani na nje ya makazi yao hali iliyo pelekea baadhi ya nyumba hizo kubomoka likiwemo kanisa la EAGT lililo kuwa limejengwa kwa thamani ya shilingi milioni hamsini.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Anaclet Frances amesema licha ya madhara yaliyo jitokeza hakuna vifo wala majeruhi kwa kuwa walichukuwa tahadhari mapema baada ya kuona dalili za mafuriko hayo nakuiomba serikali kuchimba mtalo mkubwa utakao saidia kusafirisha maji hayo kueleakea ziwa Victoria.
Akizungumzia tukio hilo kwenye kikao cha baraza la madiwani mkuu wa wilaya hiyo Bw Shaban ntarambe amewahakikishia wananchi hao kuwa atalifanyia kazi suala hilo kwa kujenga mtalo mkubwa utakao saidia kutiririsha maji hayo.
Sanjari na hayo amewataka wananchi wanao ishi mabondeni na kwenye mikondo ya maji kuhakikisha wanahana kwa hiyari ili kuepuka madhara  makubwa zaidi yanayoweza kujitokeza.


No comments:

Post a Comment