Thursday 8 March 2018

SERIKALI YAAHIDI MAZURI KWA WACHIMBAJI WADOGO WADOGO NCHINI

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akiwaeleza wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu katika Kijiji cha Bululu, kilichopo katika Kata ya Nyamtukuza Wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita juu ya umuhimu wa kufuata taratibu na sheria katika uchimbaji.

Wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu katika Kijiji cha Bululu, kilichopo katika Kata ya Nyamtukuza wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko wakati akiwa katika ziara ya kikazi Wilaya ya Nyang'wale Mkoani Geita.

Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe Hussein Nassor Amari Kasu  akizungumza na kuelezea kero ambazo wamekuwa wakizipata wachimbaji wadogo za kuondolewa kila mala kwenye maeneo ambayo wanayazindua.

Mkuu wa wilaya ya Nyang'hwale Hamim Gweyama akiwaeleza wachimbaji kufuata taratibu na sheria ambazo zimewekwa kwenye maeneo ya uchimbaji madini.

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akiwaeleza wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu katika Kijiji cha Bululu, kilichopo katika Kata ya Nyamtukuza Wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita juu ya umuhimu wa kufuata taratibu na sheria katika uchimbaji.



Serikali imesema imedhamiria kuwanufaisha wananchi kupitia rasilimali za nchi hususani sekta ya Madini hivyo wachimbaji wadogo wanapaswa kuzingatia maelekezo ya serikali ikiwemo taratibu na sheria katika uchimbaji.

Naibu Waziri wa Madini Bw DotoBiteko ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wachimbaji wadogo katika Kijiji cha Bululu, kilichopo Kata ya Nyamtukuza Wilayani Nyang'hwale Mkoani Geita.

Alisema Serikali imetenga maeneo maalum kwa wachimbaji wadogo katika mkoa wa Geita na maeneo mengi nchini huku akisisitiza kuwa kuna leseni za utafiti na uchimbaji mdogo 24 ambazo zinaisha muda wake March 30 mwaka huu katika Wilaya ya Nyang'hwale.

Amewataka wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kwa kuwa Serikali inatazama namna ya kuwapatia wachimbaji wadogo baadhi ya maeneo hayo.

Naibu waziri Biteko ameendelea kusema  kuwa serikali itatoa leseni kwa ajili ya maeneo ya uchimbaji lakini haitatoa leseni hizo kwa mtu mmoja mmoja badala yake amewasihi wachimbaji hao kuanzisha vikundi ili kupatiwa leseni hizo.

Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale Bw Hussein Kasu alimueleza Naibu waziri  kuwepo kwa tabia ya kufukuzwa  wachimbaji wadogo hata kama wanakuwa wakivumbua maeneo ambayo yanadhahau kwa madai kuwa yapo ndani ya leseni hali ambayo imewapelekea kujiona kama wao ni wakimbizi.

Hata hivyo kufuatia agizo ambalo limetolewa na Naibu waziri wa madini Bw Biteko, baadhi ya wachimbaji wamesema matarajio yao yalikuwa ni kuruhusiwa kuendelea kufanya kazi kwenye maeneo ambayo walikuwa wameanza  uchimbaji hivyo hawaafiki kuendelea kusubilia hadi tarehe ambayo wameambiwa .


Aidha  Biteko pia amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Nyang'wwale Bw Hamim Gwiyama kuitisha kikao ndani ya wiki moja kwa kuwaalika wananchi wote wenyewe vikundi ili kuwaelekeza namna bora ya kufanya kazi za uchimbaji kwa kufuata taratibu na sheria.

No comments:

Post a Comment