Saturday 29 April 2017

WANAFUNZI 11 WASHINDWA KUENDELEA NA MASOMO KUTOKANA NA KUPATIWA MIMBA WILAYANI BUKOMBE

Baadhi ya wanafunzi shule ya Msingi ya Uyovu wakiwa kwenye sherehe za kutimiza miaka Kumi tangu kuanzishwa kwa shule Hiyo


Mgeni rasimi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bukombe pamoja na msafara wakiingia kwenye viwanja vya maazimisho ya sherehe za jubilee yaliyokuwa yakifanyika kwenye viwanja vya shule Hiyo pembeni yake mkono wa kushoto ni mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Nicas Safari.

Msafara ukiingia kwenye viwanja shughuli inapofanyika.

Kwaya ya wanafunzi shuleni hapo ikiingia kutoa Burudani ya uwimbaji.

Wadau mbali mbali wakiwemo walimu pamoja na wazazi wakifuatilia kwa makini shughuli ya uwimbaji iliyokuwa ikiendelea.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe ,Nicas  Safari Mayala akijitambulisha mbele ya wanafunzi na wazazi ambao walikuwa wamefika kwenye sherehe Hizo.

 Wanafunzi wa Skauti wakionesha ukakamavu wao kwa kutengeneza mnara kwenda Juu kwa kubebana wao kwa wao.

Skauti wakivunja Tofari lililokuwa tumboni kwa mwanaskauti.

Mwalimu Mkuu wa Shule y Sekondari Uyovu, Saimon Mashauri akielezea mbele ya mgeni Rasmi Makusudi na Malengo ya kuwepo kwa sherehe ya Jubilee ya Miaka Kumi tangu kuanzishwa kwa shule hiyo.

Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Sekondari Uyovu  Josephat Waka  akielezea changamoto za watoto kukatishwa masomo kutokana na kupigwa mimba wakiwa katika kipindi cha umri mdogo.

Meza Kuu ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe pamoja na Mbunge na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo.

Vijana wa Kudesi na Kubugi wakionesha mautundu yao wakati wa sherehe ya miaka kumi ya shule ya Sekondari ya Uyovu.

Mbunge wa Jimbo Bukombe  Dotto Biteko,Akitoa neno la utangulizi na kumkaribisha Mgenu Rasmi kwaajili ya kuzungumza na wazazi wanafunzi na baadhi ya wananchi waliuzulia Hafra hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga akizungumza na wananchi waliofika kwenye Hafra Hiyo ambapo moja kati ya maagizo ambayo ameyatoa ni watuhumiwa kukamatwa ndani ya wiki inayokuja.

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe hakigawa vyeti vya pongezi kwa idara ambazo zimefanya vizuri shuleni hapo.



Wanafunzi 11 wote wakiwa wa Sekondari,sita kutoka Uyovu Wilayani Bukombe Mkoani Geita,wamekatishwa masomo yao baada ya kupata ujauzito huku baadhi ya watendaji wa Serikali Idara ya Elimu Wilayani humo wakidaiwa kugeuza mtaji matukio hayo kwa kushirikiana na wazazi,wanaume waliowapa mimba kisha kuyamaliza kimyakimya.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Sekondari Uyovu  Josephat Waka  ambaye ameibua tuhuma hizo mbele ya viongozi mbalimbali wa chama na Serikali akiwemo mkuu wa Wilaya hiyo  na Mbunge wa jimbo hilo  wakati wa Jubilee ya miaka kumi tangu ilipoanzishwa shule hiyo.

“Hadi kipindi hiki kuna mimba sita kwenye shule ya sekondari ya uyovu sisi kama bodi tumejitaidi kupeleka taarifa sehemu husika lakini taarifa ya kusikitisha kuna baadhi ya wazazi watumishi sio waaminifu wamekuwa wakishirikiana na  watu hawa ambao wamewapa watoto mimba mwisho wa siku wanatoroka mimi kama mwenyekiti wa Bodi nilikuwa nimefikilia Jambo moja endapo kama tutawapata chama cha wanasheria wanawake kuja na kutusaidia swala hili naamini tutamaliza tatizo hili maana linasumbua kwa kiasi kikubwa katika maeneo yetu”Alisema Waka.

Hata Hivyo Mwenyekiti wa Bodi ya shule ameongezea kuwa Jitihada ambazo wamekwisha kuzichukua hadi sasa ni kwamba wanampango wa kukaa na wazazi waweze kuchangia ujenzi wa hostel ambazo zinatasaidia kunusuru Mimba za watoto wa kike katika shule.

“Ndugu mwandishi najua kuwa hapa uyovu ni eneo la biashara na mala nyingi kuna mabinti ambao wanaishi mbali na maeneo haya kwa hiyo unakuta wanapanga kwenye makazi ya watu mwisho wa siku wanapopata shida wanarubunika na kujikuta wakiingia kwenye mchezo wa mapenzi hivyo jitihada kubwa tunaona sisi kama Bodi ya shule ni kukutana na wazazi na kuwaomba kuchangia ili tuweze kujenga hostel kwa kushirikiana na serikali”Alisema Waka

Mbunge wa Jimbo hilo Dotto Biteko ambaye alikuwa ameambatana na Mgeni Rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya Hiyo,amesikitishwa na taarifa hizo ambapo amechukua nafasi hiyo kuwahasa wanafunzi kuachana na tabia ya kuharakia mapenzi katika umri mdogo.

“Tumeambiwa hapa kuna mimba sita kwenye shule hii Mh Mkuu wa Wilaya Nitashangaa sana endapo kama kuna mtu amemtia  mimba mwanafunzi yupo mitaani hajachukuliwa hatua zozote za kisheria kama kuna mzazi ambaye mtoto wake amepatwa mimba na anakwenda kuonga ili Yule aliyemtia mimba mtoto wake aachiwe huru mimi inaniuma sana unakuta mtoto mdogo ametiwa mimba anaangaika na mtoto lakini mwanaume yeye anaendelea na maisha yake bila shida yoyote ,Nanyinyi wanafunzi tunawaomba msome sio uko shule na wewe unakuwa na maswala ya Bebi subilia wakati wako utafika”Alisisitiza Dotto.

Kaimu Afisa elimu wa Wilaya hiyo  Mwl Leornad Kingwa mbali na kukiri wanafunzi sita wa Sekondari hiyo kukatishwa masomo kwa ujauzito wamedai wamekwishaanza kuchukua hatua huku mkuu wa Wilaya hiyo Maganga akiagiza kufikia wiki ijayo awe amepewa orodha ya majina ya wanaume waliowapa mimba watoto hao ili achukuwe hatua haraka iwezekanavyo ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwenye vyombo vya kisheria.

“Changamoto zipo wajawazito wapo wanapatikana kiwilaya wanafunzi takribani kumi na moja wanaujauzito ingawa shule ya uyovu ndio imeonekana kuwa na wanafunzi wengi zaidi tumeshachukua hatuia taarifa zipo kwenye jeshi la polisi tayario”Alisema Kingwa.

Hata hivyo baadhi ya wazazi Julius John na Lucy Malaki pamoja na kumshukuru Mkuu wa wilaya kwa maamuzi ambayo ameyachukua pia wamewaomba watu wenye tabia za kuwakatisha masomo mabinti waliopo mashuleni kuachana na Tabia hiyo kwani  imekuwa ikisababisha kudidimiza ndoto za wasichana wengi..






No comments:

Post a Comment