Friday 21 April 2017

HAMASHAURI YA MJI WA GEITA YAVUKA LENGO UJENZI WA MADARASA MTAA WA 14 KAMBARAGE

Madarasa ambayo yapo kwenye shule ya Msingi Kambarage 14 yakionekana kukamilika kwa nje.

Kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi CCM  Kata ya Buhala hala ikikagua mradi huo katika utekelezaji wa Ilani ya chama hicho.

Daud Benson Ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Buhala hala akielezea namna ambavyo  wamerihishwa na shughuli ambazo zimefanywa na serikali kwa ushirikiano wa Diwani wa Kata Hiyo

Daud Benson Ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Buhala hala akimsisitiza Diwani wa kata hiyo  Mussa Kabese kufanya kazi kwa bidii za wananchi ili kutimiza ilani ya chama hicho.

Mwenyekiti wa kata ya Buhala hala,Fanuel Emmanuel akielezea matarajio ya kuona shughuli za maendeleo zinatekelezwa kwa wakati Katika kata Hiyo

Diwani wa Kata ya Buha hala ,Mussa Kabese Akionesha maeneo ambayo ni ya mipaka ya shule hiyo kwa Kamati ya Siasa kwenye kata Hiyo.




Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rasi Dk John Magufuli imeendelea kutekeleza ahadi zake za utekelezaji  wa miradi ya ujenzi wa shule za msingi  Kwenye mitaa na Kata Tofauti ndani ya halmashauri ya Mji wa Geita Wilayani humo, ikiwa ni juhudi za kuondoa usumbufu wa wanafunzi kutembea umbali wa kilomita ndefu .

Kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi CCM  Kata ya Buhala hala Imetembelea mradi unaoendelea katika Mtaa wa 14 kambarage,   wakitimiza matakwa ya kikatiba ndani ya chama hicho ambayo inawataka viongozi kutembelea na kujionea utekelezaji wa ilani ya uchaguzi kama ambavyo ibara ya 189 ya mwaka 2015/20 inavyosema.

Akizungumza na wajumbe waliotembelea shule hiyo mpya ambayo iko mbioni kukamilika  Diwani wa kata ya Buhala hala Musa Kabese amesema kuwa mradi huo umegharimu kiasi cha sh Milioni mia moja (100) na kwamba walitakiwa wajenge majengo matatu lakini wao wamekwenda mbele zaidi na kujenga madarasa manne.

“Wajumbe kama mnavyoona haya ni madarasa manne ambapo ujenzi huu umegharimu kiasi cha Sh,milioni Mia moja tunamshukuru Mungu kwa kuwa tumevuka malengo tuliambiwa madarasa matatu lakini sisi tumekwenda mbele tumejenga manne.”Alisema Kabese

Mwenyekiti wa CCM kata ya Buhalahala Fanuel Emmanuel alisema moja kati ya majukumu ya chama cha mapinduzi CCM ni kutekeleza ilani yake na kwamba kwa sasa uchaguzi umekwisha kumalizika ni vyema kazi zikafanyika na zikaonekana kutokana na ahadi ambazo walizitoa wakati wa kampeni kwa wananchi.

Nao baadhi ya wajumbe wamesema shule hiyo itakapokamilika na kuanza kutumika itaondoa kero ya wanafunzi kutembea umbali mrefu, huku wakibainisha maeneo ambayo bado yanakabiliwa na changamoto.

Kukamilika kwa ujenzi wa shule hiyo kutapunguza changamoto ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata elimu pamoja na ajali ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara

No comments:

Post a Comment