Thursday 27 April 2017

WAWILI WATUMBULIWA NA WENGINE KUSIMAMISHWA KAZI KWAAJILI YA KUPISHA UCHUNGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Elisha Lupuga akisoma maadhimio ya Baraza Juu ya kuwasimamisha Watumishi wawili ambao wamekiuka misingi  ya ajira.

Diwani wa Kata ya Nyamalimbe Jeremia Ikangala Akiunga Mkono maadhimio ya baraza la madiwani la kuwafukuza kazi watumishi na kuwasimamisha watumishi wengine kwaajili ya kupisha uchunguzi.

Baadhi ya madiwani wakifuatilia kikao maadhimio ya Baraza hilo.

Diwani wa Kata ya Nyarugusu Swalehe Juma akielezea juu ya hatua ambayo imechukuliwa kuwa ni mfano wa kuingwa kwa watendaji ambao wamekuwa na tabia za namna kutokutimiza majukumu ambayo wanatakiwa kuyafanya.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ,Ali Kidwaka akisikiliza maadhimio ambayo yalikuwa yakitolewa na mwenyekiti wa Halmashauri hiyo.


Baraza la Madiwani halmashauri ya wilaya ya Geita Mkoani humo kupitia mamlaka ya nidhamu ya watumishi imewafukuza kazi watumishi wawili wa halmashauri hiyo kwa utovu wa nidhamu na utoro kazini kwa muda mrefu. Na kuwasimamisha kazi watumishi wengine wawili kwa lengo la kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili.

Akitanganza uamuzi huo mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Elisha Lupuga, baada ya baraza hilo kujiegeuza kuwa kamati ya nidhamu  kwa dharula  amesema hatua hiyo ni kuonesha namna gani watumishi wanatakiwa kufuata nidhamu kazini.

Mwenyekiti huyo amewataja waliofukuzwa kazi kuwa ni Nzalagaza Nyanda  ambaye alikuwa  idara ya utawala na Alphonce Mgimwa ambae alikuwa ni muuguzi katika zahanati ya  Furu ambae aliondoka kazini siku 50 bila taarifa .

Waliosimamishwa kwaajili ya uchunguzi ni mhandisi wa maji Halmashauri hiyo Rahel Antony ambae amesimamishwa kwaajili ya kupisha uchunguzi wa mradi wa maji wa Chankorongo ambao umesuasua kutokumalizika kwa miaka mingi na Denis Nyasaba ambae ni afisa ugavi wa halmashauri ambaye anachunguzwa kwa mikataba mibovu ya miradi.

“Kwa mujibu wa sheria za kanuni ya arobaini na mbili jedwali la kwanza sehemu A kipengele cha nne cha kanuni za utumishi wa uma  za mwaka 2003 na kanuni ya 57 kifungu kidogo cha kwanza  cha kanuni za utumishi wa uma ambapo namba F 16 kifungu kidogo cha kudumu cha mwaka 2009 watumishi hawa kuwa watoro kazini na kwamba wanaposhindwa kufika ofisini ndani ya siku tano sheria inatambua kuwafukuza kazi kwa hiyo natangaza kuanzia leo watumishi  hawa wamefukuzwa kazi kwa kuzingatia mamlaka ya kazi za uma “Alisisitiza Lupuga.

Madiwani wa Kataza Bukondo  na Lwamgasa John Maguru na Dotto Kaparatus amepongeza hatua hiyo huku wakiwataka watumishi kufuata kanuni na taratibu za mikataba ya ajira na pia kuwa waaminifu pindi wanapopatiwa  kazi.


IMEANDALIWA

No comments:

Post a Comment