Wednesday 26 April 2017

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA KIJIJI CHA BUSINDA MKOANI GEITA AZUA TAHARUKI



Hofu  imetanda kwa wananchi wa kitongoji cha Sikalibuga kijiji cha Businda kata ya Ushirombo wilayani Bukombe mkoani Geita kwa kuongozwa na wenyeviti wawili katika  kitongoji kimoja  kinyume na sheria.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya serikali wilayani humo kumuondoa aliyekuwa mwenyekiti wa kitongoji hicho  toka mwaka 2015  kwa sababu mbalimbali zinazo eleza kuwa ni matumizi mabaya ya madaraka.

Akizungumza katani hapo Diwani wa kata hiyo ya Ushilombo Bw. Lameck Warangi amemtaja mwenyekiti aliyeondolewa katika kiti cha uongozi tangu mwaka 2015 kuwa ni Malisera John mkazi wa Sikalibuga.

Bw. Warangi amesema chanzo kilichosababisha kiongozi huyo kuondolewa  ni pamoja na kutuhumiwa kwa makosa matatu ambayo ni kuuza eneo la kijiji bila kufuata uataratibu wa kisheria,matumizi mabaya ya madaraka na kushindwa kuitisha mikutano ya hadhara  kisheria tangu alipo chaguliwa .

Kwa upande wa kaimu mwenyekiti aliye chaguliwa na wananchi katika eneo hilo Bw. Mandago Singu ameelaza kuwa amekutana na changamoto nyingi tangu achaguliwe kukaimu kitongoji hicho kwani mwenyeki wa aliyekuwepo amegushi nyaraka za serikali ikiwa ni pamoja na kuchonga mhuri  feki na amekuwa akifanya kazi kama mwenyekiti haliyakuwa  ameondolewa  kisheria .


Sambamba na hilo Bw. Singu ameiomba serikali yenye dhamana ya kulishughulikia jambo hilo ifanye haraka iwezekanavyo ili kuepuka matatizo yasiyo kuwa yalazima ambayo yanaweza kujitokeza kijijini humo.

No comments:

Post a Comment