Thursday 20 April 2017

UVUVI HARAMU WAKOMESHWA WILAYANI CHATO MKOANI GEITA



Mwenyekiti wa watunza mazalio na makulio ya samaki  Bashiri Manampa  kutoka  Mwaro wa Nyamilembe wilayani Chato mkoani Geita amewashukuru wenyeviti wenzake wa miaro ya buhungu na nyakakarango kwa kufungua mipaka  ili kukomesha uvuvi haramu ndani ya ziwa victoria.
Akizungumza ofisini kwake  Bw. Manampa amesema ni muda mrefu amekuwa akiwaomba wenyeviti hao kufungua mipaka waliyokuwa wamejiwekea  hali ambayo ilipelekea wavuvi haramu kutumia  mipaka hiyo kujificha na kukwepa doria ya majini.

Katika hatua nyingine Bw. Manampa ameongeza kuwa kutokana na ushirikiano huo  watapunguza au kuondoa suala la uvuvi haramu ambalo limekuwa  na changamoto   nyingi  wilayani humo.

Aidha hivi karibuni waziri wa kilimo ,uvuvi na mifugo dk charlse tizeba alifika wilayani humo na kuzungumza na wananchi wa eneo hilo ambapo ametoa onyo kali kwa watu wanao jihusisha na uvuvi haramu ikiwa ni pamoja na kuongeza adhabu kwa mtu atakae bainika anajihusisha na vitendo hivyo


 Baadhi ya wananchi wa nyamirembe na nyakakarango bw: ganyanka  matele  na edward magafu wameipongeza serikali kwa jitihada za kupambana na matumizi ya zana haramu za uvuvi ikiwa ni njia ya kutokomeza uvuvi haramu hapa nchini. 

No comments:

Post a Comment