Monday 3 April 2017

MAJENGO YA KUSIKILIZIA KESI ZA WATOTO NI MUHIMU KWENYE MAHAKAMA

Wanasheria wakuu wa Serikali, waendesha mashitaka,Makarani wa Mahakama na Askari polisi wa kitengocha upelelezi na dawati la Jinsia kutoka wilaya zote zaMkoa wa Geita wakiwa kwenye mafunzo.

Wakili wa serikali Mkoani Geita Bw Emily Kiria ,akielezea  mikakati iliyopo baada ya kupatiwa semina  hiyo.

Meza kuu ikiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Geita  Mwl Herman Kapufi(aliyekaa katika katika)


Wanasemina wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Mkuu wa wilaya.


Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akisisitiza Juu ya serikali kuona umuhimu wa kuwa na vyumba vya kutosha kwaajili ya kusikiliza madai ya watoto.

Mratibu wa Miradi Plan International Geita  Maxmillian Mtigwa akizungumzia dhamira ya shirika hilo kufadhiri semina hiyo.
Upungufu wa majengo ya kusubiria uendeshwaji wa Kesi za watoto umetajwa kuwa miongoni mwa changamoto zinazosababisha watoto wengi kupata hofu na kushindwa kutoa ushirikiano na ushaidi katika Kesi zinazowahusu.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Ezekiel Kyunga, aliyewakilishwa na Mkuu wa wilaya ya Geita Bw Herman Kapufi wakati wa kufunga Semina ya Wanasheria wakuu wa Serikali, waendesha mashitaka, Makarani wa Mahakama na Askari polisi wa kitengo cha upelelezi na dawati la Jinsia kutoka wilaya zote za Mkoa wa Geita.

Bw Kapufi alisema  watoto wengi hupata hofu pale wanapoona idadi kubwa ya Askari mahakamani na kwamba lipo tatizom kwa wananchi kushindwa kutoa ushirikiano wa ushahidi mahakamani.

"Upungufu wa majengo ni sababu ambayo inaonekana kuwafanya watoto kuwa waoga kwani wanapopelekwa polisi wanapowaona tu askali wanakuwa na uogo mimi nitaandika barua kwenye mamlaka usika ili kushughulikia tatizo hili"alisema Kapufi

Kwa upande wake Wakili wa serikali Mkoani Geita Bw Emily Kiria amesema sheria ya watoto ya mwaka 2009 haijaeleweka vizuri kwa wananchi na hivyo. 

No comments:

Post a Comment