Monday 10 April 2017

SERIKALI KUTOA ELIMU YA KUJIKINGA NA KIFUA KIKUU KWA WACHIMBAJI MADINI



Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsi Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Hamis kigwangalla akijibu hoja mbalimbali za wabunge katika kikao cha nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma.
Serikali kupitia Halmashauri zilizo katika maeneo ya migodi imeanza kuweka mikakati ya kudhibiti magonjwa ya Kifua kikuu na Silicosiskwa kutoa Elimu kwa wachimbaji  wa madini ikiwemo kujikinga na vumbi na kutumia njia sahihi za uchimbaji.

Hayo yamesemwa na Naibu Naibu WazirwAfya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Khamis Kingwangalla leo Bungeni Mjini Dodoma wakati wa Maswali na Majibu.

“Tanzania inafahamu changamoto ya uwepo wa magonjwa  haya ya kifua kikuu na Silicosis katika maeneo ya wachimbaji, kwa upande wa Kifua kikuu tatizo hili ni kubwa lakini kuwekuwepo na ripoti za wagonjwa wachache wa Silicosis  katika hospitali za Serikali ikiwemo Kibong’oto”,Alibainisha Mhe.Kigwangalla.

Ameeleza kuwa kupitia ufadhili wa Mfuko wa Dunia wa kupambana na Magonjwa ya UKIMWI,Kifua Kikuu, na Malaria wa Global Fund to Fight AIDS,Tuberculosis na Malaria nchi kumi wananchama wa jumuiya ya SADC ikiwemo Tanzania ziko katika utekelezaji wa mpango wa kudhibiti kifua kikuu na magonjwa ya mfumo wa hewa yatokanayo na uchimbaji madini ikiwemo Silicosis.

Aidha katika mpango huo kuna afua  itakayo shughulika na sera  za udhibiti wa vumbi katika maeneo ya wachimbaji ambayo itawabana wachimbaji kudhibiti vumbi wakati wa shughuli za uchimbaji.


“Serikali itaongeza wigo wa huduma katika vituo vya afya kwenye maeneo yaliyoathirika  ikiwemo Mkoa wa Geita ili vituo viwe na uwezo wa kuchunguza na kutibu magonjwa haya na kuwajengea uwezo wataalamu wa afya katika kuhudumia wagonjwa katika maeneo ya migodi”Alisisitiza Mhe. Kingwangalla.

No comments:

Post a Comment