Monday 10 April 2017

WANACHAMA WA CCM GEITA WATAKIWA KUWA NA UMOJA NA UPENDO HILI KUIMARISHA CHAMA HICHO.

Naibu katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Bara Rodrick  Mpogolo ,akizungumza na wajumbe wa chama Hicho Mkoani Geita wakati alipokuwa akitoa maelekezo kwa viongozi ngazi za kata,mitaa vijiji na  Wilaya. 

Naibu katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Bara Rodrick  Mpogolo akisisitiza juu ya wanachama kuwa na umoja.


Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Mkoani Geita Joseph Kasheku Msukuma akielezea mwelekeo wa chama ndani ya Mkoa mbele ya Naibu Katibu Mkuu Bara.

Katibu Mwenezi wa chama cha mapinduzi Wilaya ya Geita Jonathan Masele aliyevaa shati la kitenge pamoja na katibu wa wazazi wilaya ya Geita wakiserebuka na "ccm mbele kwa mbeleee acha waisome namba heeeee".

Wajumbe wakifatilia kwa kikao.






Katibu wa CCM Mkoa wa Geita ,Adam Ngallawa akielezea shughuli ambazo zimeendelea kufanywa na chama.

Moja kati ya wanachama wakubwa wa chama cha Demokrasia na maendeleo Mkoani Geita akikabidhi kadi yake kwa Naibu katibu Mkuu na kujiunga na chama cha CCM.

Akielezea sababu ya kuondoka CHADEMA.

Naibu katibu Mkuu akimpongeza moja kati ya wananchi ambaye ameamua kujiunga na CCM.


Naibu katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Bara Rodrick  Mpogolo amekutana na wajumbe wa  sekretalieti za chama Wilaya zote zilizopo Mkoani Geita  na kuwasisitiza wananchama hao kuwa na umoja na upendo ndani ya chama huku wakiwa na umoja kwenye shughuli ambazo zinausiana na chama hicho.

Mpogolo amesisitiza hayo wakati wa kikao cha maelekezo kilichofanyika kwenye  ukumbi wa halmshauri ya mji wa Geita mjini humo,alisisitiza kuwa ni wakati wa wananchama kuakikisha wanajenga umoja hili chama hicho kuwa imara na chenye nguvu ambacho kitaendelea kuchukua .

“Lazima kwanza wanaccm tubadirike tuanze kuwa na umoja ndani ya chama chetu tuachane na unafiki,majungu chuki na fitina maana hata imani ya chama chetu kinaamini kuwa swala la umoja na usawa ni msingi ambao upo ndani ya chama chetu”Mpogolo aliwasisitiza wanachama.

Aliongeza kuwa endepo kama wanachama wataeshimiana na kupendana   hakika chama kitaendelea kuleta mageuzi makubwa ndani ya chama na kwamba kazi iliyopo ni kuongeza wanachama ndani ya CCM  na kwamba lazima kila mwanachama awe na uwezo wa kushauri kwa watu kujiunga na chama hicho.

Aidha kwa Upande Mwingine amehimiza swala la maadili na kupinga vikali maswala ambayo yanaweza kukichafua chama hicho kama mambo ya Rushwa  na kutokutambua haki za kila mwanachama ambaye yumo ndani ya chama hicho.

Katibu pia amewataka viongozi wa chama kusimamia ilani ya uchaguzi katika maeneo yao kwa weledi mkubwa ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Mkoani Humo Joseph Kasheku Msukuma amemwakikishia  Naibu Katibu Mkuu kuyafanyia kazi maelekezo ambayo ameyatoa huku akiwasisitiza viongozi kuzingatia misingi ya haki na usawa kwa kuwatumiakia wananchini na kwamba yale ambayo yamesemwa inawezekana endepo kwa kila kiongozi na mwanachama   hakitimiza wajibu wake.

No comments:

Post a Comment