Wednesday 19 April 2017

WATATU WAKAMATWA KATIKA MSITU ULIOHIFADHIWA WAKIKATA MITI



Watu watatu wakazi wa  mamlaka ya mji mdogo wa katoro wilayani na mkoani Geita wamekamatwa baada ya kukutwa katika msitu ambao umezuiwa kufanyika shughuli za kibinadamu huku  wakiwa wanakata miti.
Wakizungumza watu hao ambao wametambulika kwa majina ya Paskali Songano , John Zakaria  na  Lukas Philipo wote wakazi  wa mtaa wa mtoni katika mamlaka ya mji mdogo wa katoro ambapo wamesema kuwa  waliingia katika msitu huo kwa lengo la kukusanya magogo kwa ajili ya kuyatumia katika shughuli  za uchomaji  wa  matofari .

Sanjari na hayo watu hao wamesema kuwa kabla ya kuingia katika msitu huo walipita kwa mwenyekiti wa eneo  hilo na  aliwaruhusu  kuingia katika msitu huo kuchukua magogo ya visiki vya miti  kwa kuchangia kiasi cha pesa  taslimu shilingi elfu ishirini na kiongozi huyo aliwapatia  stakabadhi ya halmashauli ya wilaya ya geita kama kielelezo pindi wapatapo  matatizo msituni humo.

Kwa upande wake mlinzi wa msitu huo  alie husika kuwakamata watu hao Bw.Zabroni Peter ameeleza kuwa amewakuta watu hao wakiwa  wanakata miti  kwakutumia shoka walizo kuwa nazo  na siyo kwamba walikuwa wanakusanya magogo kama wanavyo eleza wao. 

Aidha mwenyekiti wa mtaa huo Bw. Masunga Mbishi amekiri kuwapatia kibali cha kuwaruhusu watu hao kuingia katika msitu huo kwa lengo la kuchukua magogo na siyo kukata miti kama inavyo elezwa .

Bw.  Masunga amesema  watu hao waliokamatwa na mlinzi wa msitu huo hawana hatia kwasababu yeye ndiyo aliyewapatia ruhusa ya kuingia katika eneo hilo kutokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya miti ambayo imeharibiwa vibaya na watu wasio julikana.

Mpaka sasa watu hao wameachiwa huru.

No comments:

Post a Comment