Wednesday 10 August 2016

WAZIRI WA ZAMANI WA HABARI WA CHINA AWAPIGA MSASA WAKUU WA VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI



Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya Watu wa China, Bw. Zhao Qizheng akimuonesha Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Hassan Abbas kitabu cha Shanghai Pudong Miracle kinachoonesha jinsi mji wa Shanghai ulivyotoka kuwa mji wa hali ya chini hadi kufikia mji wa kisasa na wenye maendeleo, wakati wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu wa masuala ya Mawasiliano Serikalini baina ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini na Waziri huyo leo Jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya Watu wa China Zhao Qizheng akiongea na Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini kuhusu umuhimu wa Serikali kuwasiliana kimkakati na wananchi na namna bora ya kuwasilisha taarifa kwa jamii, wakati wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu wa masuala ya Mawasiliano Serikalini, leo Jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Hassan Abbas.




Baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini wakimsikiliza Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya Watu wa China, Zhao Qizheng, wakati wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu wa masuala ya Mawasiliano Serikalini, Leo Jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya Watu wa China Zhao Qizheng na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Hassan Abbas wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini, wakati wa kikao kazi cha kubadilishana uzoefu wa masuala ya Mawasiliano Serikalini, leo Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Hassan Abbas akiongea na baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi baina ya Waziri wa Zamani wa Habari wa Jamhuri ya watu wa China Zhao Qizheng na Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini.


No comments:

Post a Comment