Wednesday 3 August 2016

WAFANYABIASHARA WADOGO WA SOKO LA NYANKUMBU MKOANI GEITA WAMLALAMIKIA DIWANI WA KATA HIYO






































Diwani wa Kata ya Nyankumbu akiendesha zoezi la kutoza ushuru kwa baadhi ya wafanyabiashara



 Baadhi ya wanunuzi wa Bidhaa katika Soko hilo

Wafanyabiashara  wadogo wa mboga mboga na matunda katika Soko la Nyakumbu lililopo Kata ya Nyakumbu Wilayani na Mkoani Geita,wamelalamikia kitendo cha Diwani wa Kata hiyo Bw.Michael Kapaya kuwatoza  Ushuru wa Sh.200  kwani hivi karibuni kumekuwepo na agizo kutoka kwa Rais John Magufuli la kutokuwabughuzi wafanyabiashara wadogo.

Wakizungumzia sakata hilo baadhi ya wafanyabiashara Bi.Thabiza Shuli ,Suzana Enock na Bw. Julius Charles ambao wanafanya biashara katika soko hilo wamesema  kuhusiana na kuchangia gharama za usafi wa soko wamekuwa wakilipa lakini hawaoni usafi unaofanyika hali ambayo imewasababisha kuwa wagumu wa kutoa ushuru huo na sababu nyingine wakieleza ni diwani kuingilia majukumu ambayo si ya kwake kwani majukumu hayo ni ya mtendaji wa Kata au Mtaa husika.

Katibu wa Soko hilo Bw.Philimon Charles,ameelezea kuwa kutokana na suala hilo yeye kama kiongozi anajua kuwa nafasi ya Diwani ni kuhakikisha anahimiza watu kutoa ushuru lakini yeye sio kusimamia zoezi la kuwatoza ushuru wafanya biashara hao.

Kwa upande wake Diwani wa kata hiyo Michael Kapaya  ameeleza kuwa kufikia uamuzi huo ameshakutana na Mtendaji na Viongozi wengine na mwisho wa siku aliamua kufanya hivyo kwa lengo la kutoza fedha hizo ili usafi ufanyike katika soko hilo.


Mkurugenzi wa halmashauri ya mji mhandisi Modesti Hapolinali amesema kuwa  Diwani jukumu lake kubwa ni kuwahimiza wafanyabiashara kutoa ushuru na sio kutoza fedha na kwamba katika soko hilo kuna  watu wamekwisha wekwa kwa ajili ya kutoza fedha na wanahusika ni wale ambao wana meza za biashara ndani ya soko hilo ndio wanahusika kutozwa fedha lakini sio wale ambao wapo nje ya soko

No comments:

Post a Comment