Friday 19 August 2016

WATU WAWILI MKOANI GEITA WAUWAWA KWA KUCHOMWA MOTO NA WATU WASIOJULIKANA



Watu  wawili wameuawa kwa kuchomwa moto na watu wasiojulikana kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wavuvi haramu waliokuwa wakifanya shughuli za uvuvi kwa kutumia sumu katika ziwa Victoria na kisha watu hao kubomoa  nyumba za mrehemu hao hali ambayo imewalazimu askari kutumia silaha kali ili kuwatawanya watu hao.

Tukio hilo limetokea majira ya saa kumi usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Nyamalele Kata ya Nkome mkoani Geita ambapo marehemu mmoja aliyefahamika kwa jina la Franco Mganda  mkazi wa kijiji cha Nkome na mwingine ambaye bado jina lake halijajulikana wameuwawa na wananchi kisha kuteketezwa kwa moto.

Wakizungumza baadhi ya mashuhuda waliofika kushuhudia tukio hilo Bw.Thobias Kapuli na Bw.Tom Samsoni wamesema kuwa marehemu aliyefahamika kwa jina la Franco alikuwa ni mwendesha pikipiki ambaye alikuwa ameenda kubeba samaki wanaodaiwa kuwa walikuwa wamevuliwa kwa njia haramu ndipo akiwa njiani alikutana na watu wasiojulikana wakaanza kuwashambulia na hatimae kupoteza maisha.

Hata hivyo mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl.Herman Kapufi amefika katika eneo la tukio na kulaani kitendo hicho huku akiwataka wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake kutoa taarifa katika vyombo husika ili  vyombo hivyo viweze kushughulikia.
Aidha Kapufi amevitaka  vyombo vyote vinavyohusika na kutoa haki kwa jamii ikiwemo Polisi na Mahakama kutenda haki kwa wananchi ili kuondoa hasira kwa wananchi pindi wanapokuwa hawajatendewa haki.


Katika hatua nyingine Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Mponjoli  Mwabulambo amethibitisha kutokea  kwa  tukio  hilo.

No comments:

Post a Comment