Monday 8 August 2016

RASMI, SASA PAUL POGBA NI MCHEZAJI WA MANCHESTER UNITED

Paul Pogba akiwa na jezi ya Manchester United kwa mara ya kwanza baada ya kukamilisha usajili wake usiku wa kuamkia leo 

KLABU ya Manchester United imekamilisha uhamisho wa kiungo wa kimataifa wa Ufaransa, Paul Labile Pogba kwa dau la rekodi ya dunia, Pauni Milioni 100 kutoka Juventus ya Italia.
Kiungo huyo aliyekuwa anatakiwa na timu nyingi kubwa duniani, ikiwemo Real Madrid, aliwasili kutoka Juventus jana na kujiiunga na klabu yakzamani, ambayo aliiacha mwaka 2012.

Pogba mwenye umri wa miaka 23 anatarajiwa kuvaa jezi namba 6 na amesaini Mkataba mnono wa miaka mitano kwa mshahara wa Pauni 290,000 kwa wiki kufanya kazi chini ya kocha Mreno, Jose Mourinho. 
Kuna kipengele pia cha kuongezwa mwaka mmoja katika Mkataba huo.

USAJILI WA WACHEZAJI 10 GHALI ZAIDI DUNIANI 

Paul Pogba - Juventus kwenda Man United Pauni Milioni 100 
Gareth Bale - Tottenham kwenda Real Madrid Pauni Milioni 86 
Cristiano Ronaldo - Man United kwenda Real Madrid Pauni Milioni 80 
Gonzalo Higuain - Napoli kwenda Juventus Pauni Milioni 76 
Neymar - Santos kwenda Barcelona Pauni Milioni 72
Luis Suarez - Liverpool kwenda Barcelona Pauni Milioni 63 
James Rodriguez - Monaco kwenda Real Madrid Pauni Milioni 60 
Angel di Maria - Real Madrid kwenda Man United Pauni Milioni 60 
Kaka - Milan kwenda Real Madrid Pauni Milioni 56
Kevin De Bruyne - Wolfsburg kwenda Man City Pauni Milioni 55 
Akizungumza na tovuti ya klabu hiyo baada ya kusaini, Pogba alisema: "NIna furaha kujiunga tena na United. Imekuwa klabu yenye nafasi maalum katika moyo wangu wakati wote na ninaangalia mbele kuelekea kufanya kazi na Jose Mourinho. 

"NImefurahia maisha yangu nikiwa na Juventus na nina kumbukumbu fulani nzuri za klabu kubwa na wachezaji ambao ninaweza kuhesabu kama marafiki. Lakini nafikiri ni wakati mwafaka kurejea Old Trafford. 

"Wakati wote nafurahi kucheza mbele ya mashabiki na siwezi kusubiri kutoa mchango wangu kwenye timu. Hii ni klabu sahihi kwangu kushinda kitu chochote nachotumai kwenye mchezo,".

Kocha Jose Mourinho alimsifu Pogba na akasema anaamini atadhuhirisha thamani yake katuika urejeo wake kwenye klabu, akisema: "Paul ni mmoja kati ya wachezaji bora duniani na atakuwa mtu muhimu katika timu ya United nayotaka kujienga hapa. 

"Ni mwepesi, ana nguvu, anafunga mabao na anausoma mchezo vizuri kuliko wachezaji wengi. Akiwa ana umri wa miaka 23, ana nafasi ya kuifanya hiyo nafasi (kiungo) iwe ya kwake kwa miaka mingi hapa,"alisema Mourinho.

No comments:

Post a Comment