Tuesday 16 February 2016

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA MABALOZI 3 KATIKA WIZARA YA MAMBO YA NJE,USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, KIKANDA NA KIMATAIFA.

             
         
               Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. john pombe magufuli amefanya uteuzi wa mabalozi 3 katika wizara ya mambo ya nje, ushirikiano wa afrika mashariki, kikanda na kimataifa. Magufuli pia amefanya uteuzi wa makamishna 4 wa jeshi la polisi na kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA).

Taarifa ya katibu mkuu kiongozi balozi Ombeni Sefue, imewataja mabalozi walioteuliwa kuwa ni Dkt. Asha-rose Mtengeti Migiro, Mh Mathias Meinrad Chikawe na Dkt. Ramadhan  Dau.
Vituo vya uwakilishi kwa mabalozi hawa vitajulikana baada ya taratibu husika za kidiplomasia kukamilika.

Kwa upande wa makamishna wa polisi, balozi Sefue amewataja walioteuliwa kuwa ni:
naibu kamishna wa polisi Simon Nyakoro Sirro ambaye amepandishwa cheo kuwa kamishna wa polisi, na ameteuliwa kuwa kamanda wa polisi kanda maalum ya dar es salaam. kamishna Sirro anajaza nafasi iliyoachwa wazi na kamishna mstaafu Suleiman Kova.

Naibu kamishna wa polisi Albert Nyamuhanga ambaye amepandishwa cheo kuwa kamishna wa polisi na ameteuliwa kuongoza idara ya fedha, utawala na lojistiki.
 Kamishna nyamuhanga anajaza nafasi iliyoachwa wazi na kamishna wa polisi Clodwing Mathew Mtweve aliyeteuliwa kuwa katibu tawala wa mkoa wa mwanza.

Naibu kamishna wa polisi Robert Boaz Mikomangwa ambaye amepandishwa cheo kuwa kamishna wa polisi na ameteuliwa kuongoza idara ya intelijensia. 

Kamishna Mikomangwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na kamishna Valentino Mlowola aliyeteuliwa kuwa kaimu mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (takukuru).
Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Nsato Marijani Mssanzya ambaye amepandishwa cheo kuwa kamishna wa polisi na ameteuliwa kuongoza idara ya mafunzo na operesheni. 

Kamishna msanzya anajaza nafasi iliyoachwa wazi na kamishna wa polisi Paul moses Chagonja aliyeteuliwa kuwa katibu tawala wa mkoa wa katavi.

aidha, Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA). 

kabla ya uteuzi huu Dkt. Kipilimba alikuwa mkurugenzi wa menejimenti ya udhibiti (director of risk management) katika benki kuu ya Tanzania na hivyo Dkt. kipilimba anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Dikson Maimu ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.


teuzi zote zimeanzia jana tarehe 15 februari, 2016

No comments:

Post a Comment