Monday 22 February 2016

JESHI LA ZIMA MOTO MKOANI GEITA LIMEENDELEA KUTOA ELIMU YA MATUMIZI YA KIFAA CHA KUZIMIA MOTO (FIRE EXTINGUISHER)


   Fire extinguisher(Vifaa vya kuzimia moto)
Kutokana na baadhi ya magari ya kusafirisha abiria kuwaka moto na kusababisha ajali jeshi la zima moto  mkoani  Geita limeendelea kutoa elimu kuhusiana na matumizi ya kifaa cha kuzimia moto (fire extinguisher) katika magari  ili kuzuia ajali za moto katika magari yao.


Storm habari  imezungumza na mkufunzi wa mafunzo hayo wa jeshi la zima moto Ibrahimu Kamonja ambapo amesema kuwa  lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwasaidia madereva wote wasiojua matumizi ya kifaa hicho ili kuwasaidia wapatapo tatizo hilo.

Kwa upande mwananchi  aliyeshuhudia mafunzo hayo musa kitinde amesema utoaji huo wa mafunzo ni mzuri na utawasaidia madereva hao kujua jinsi ya kutumia kifaa  hicho pindi wapatapo ajali zitokanazo na moto katika magari yao.

Hata hivyo mmoja wa madereva hao Musa James amesema kuwa ameipokea vizuri elimu hiyo na kwamba ataifanyia kazi baada ya kuipata.

Mwenyekiti wa chama hicho cha madereva mkoani faustine john amelishukuru jeshi la zimamoto mkoani hapa  kwa kuendelea kutoa mafunzo kabla ya kutoa adhabu.

No comments:

Post a Comment