Wednesday 24 February 2016

BINTI WA MIAKA MITATU ABAKWA NA KUNYONGWA HADI KUPOTEZA MAISHA.



Mtoto mwenye umri wa miaka 3 na miezi 4 Mariam Deogratius mwanafunzi wa shule ya awali ya Makoko iliyopo katika Manispaa ya Mji wa Musoma mkoani Mara, amebakwa kisha kunyongwa hadi kupoteza maisha  na mtu asiyejulikana Usiku wa kuamkia leo.




Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara kamishna msaidizi Philllip Kalang amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa Jeshi la Polisi linafanya Msako kuhakikisha Mhalifu anapatikana.

No comments:

Post a Comment