Friday 26 February 2016

AGIZO LA RAISI MAGUFULI LAANZA KUTEKELEZWA, WAZIRI MAHIGA ARUDISHA FOMU.


        Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na                                             Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga.

Baada ya waziri mkuu kutaja majina ya mawaziri wanne na naibu waziri mmoja ambao hawajarudhisha fomu za Sekretariati ya maadili ya umma na kutakiwa wawe wamerejesha fomu hizo kabla ya  saa kumi na mbili jioni ijumaa ya leo mpaka sasa ni waziri mmoja aliyetii agizo hilo

Aliyerudisha fomu hizo ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambapo amekiri kuwa ni kweli alikuwa hajarudisha fomu hizo kutokana na majukumu ya kazi yaliyokuwa yamembana

Waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga yeye  ameshangaa jina lake kutajwa wakati tayari ameshazirudisha fomu hizo. Amesema hivi sasa  ameelekea ofisi za Sektretariati ya maadili kuwasilisha malalamiko yake

Naibu Waziri wa  Nchi (OMR – Mazingira), Bw. Luhaga Mpina yeye amesema kuwa atawahisha kurudisha fomu hizo kabla ya saa kumi na mbili jioni.

No comments:

Post a Comment