Wednesday 24 February 2016

WIZARA YA NISHATI NA MADINI KUDHIBITI TATIZO LA MILIPUKO LIANALOENDELEA KWA BAADHI YA KATA MKOANI GEITA.

       Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, (wa kwanza kushoto), akiongozwa na              Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme wa TANESCO  pamoja na wafuasi wengine.

Mbunge wa geita mjini Mh Costantine Kanyasu 

Wananchi wa kata ya mtakuja mtaa wa Nyamalembo,  Katoma na Kompaund,  wamefikisha malalamiko yao kwa Naibu Waziri wa nishati na madini,mh Dr.Medadi Kalemani juu ya nyumba zao kuendelea kubomoka kutokana na upasuaji wa miamba unaofanywa na kampuni ya uchimbaji wa madini ggm mkoani Geita.


Wakizungumza katika  ofisi za serikali ya mtaa wamesema kuwa ni vyema kwa naibu waziri kuangalia uwezekano wa kuhakikisha kuwa wanadhibiti swala la milipuko ambayo imekuwa ikitokea mara kwa mara na kusababisha athari zikiwemo za kiafya na kuharibika kwa majengo.
Aidha Dr,Medadi  Kalemani amewaomba wananchi kuwa wavumilivu na kwamba swala hilo kuaniza jumatatu ya wiki ijayo litafanyiwa kazi  na wizara hiyo kwa kupitia mtafiti wa serikali.

Katika hatua nyingine  mbunge wa geita mjini Mh Costantine Kanyasu amemshukuru  naibu waziri kwa kufika na kujionea namna na jinsi ambavyo wananchi wamekuwa wakiathirika kutokana na milipuko hiyo.

No comments:

Post a Comment