Thursday 25 February 2016

MGODI WA GEITA GOLD MINE(GGM) WALALAMIKIWA NA BAADHI YA WAKAZI WA MKOA WA GEITA.


Mgodi wa Geita Gold Mine(GGM)

Wakazi wa mitaa ya Nyamalembo ,Compound na Katoma mkoani Geita wameulalamikia mgodi wa Geita gold mine (GGM) kutokana na kuweka bikoni katika maeneo ya makazi yao zikionyesha kuwa eneo hilo ni mali ya mgodi huo hali ambayo imesababisha wananchi hao kushindwa kuendelea na shughuli zao za maendeleo.

Hayo yamebainishwa leo na wakazi wa maeneo hayo katika ziara ya naibu waziri wa nishati na madini alipotembelea maeneo hayo ili kujionea adha hiyo huku wakimuomba kulichukulia hatua za haraka  jambo hilo.

Kwa upande wake kaimu Afisa mahusiano wa mgodi huo Bw.Simon Shayo amesema kuwa kampuni hiyo haitambui madai hayo jambo ambalo limewashangaza wanachi wa maeneo hayo kutokana na kuzuiwa kufanya shughuli zao kwa muda mrefu.

Hata hivyo baada ya afisa huyo kukana kuwa kampuni haitambui zuio hilo naibu waziri wa nishati na madini Mh.Medadi Kalemani amewaagiza wananchi wamaeneo hayo kuendelea na shughuli zao huku akidai kuwalipa fidia wale waliokuwa wakidai kuzuiwa kufanya shughuli zao pindi mgodi utakapohitaji maeneo hayo.


Aidha ameongeza kuwa wananchi wanapaswa kushirikiana na viongozi kushughulikia suala la maendeleo kwani kufanya hivyo itasaidia kuongeza chachu ya maendeleo mkoani hapa na taifa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment